Baadhi
ya wafanyakazi wa Kampuni ya Benson Security Systems na AfriTrack
wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuzindua mfumo wa kimtandao wa
kudhibiti vyombo vya usafiri jijini Arusha.
Na.Vero Ignatus,Arusha
Teknolojia
ambayo itakayotumia mtandao wa mawasiliano wa internet imezinduliwa na
Kampuni ya Benson ya jijini Arusha ikishirikiana AfriTrack ya jijini Dar
es Salaam yenye uwezo wa kuthibiti wizi wa pikipiki na vyombo vya moto
Miqdaad
Kassam ni Mkuu wa Uendeshaji wa Kampuni ya Benson, amesema wakati wa
uzinduzi huo kuwa,kwa kutumia teknolojia hiyo,pikipiki ikiibiwa,
itapatikana kwa kuwa itaonekana eneo iliyopo
“Ni
teknolojia rahisi itakayodhibiti wizi wa pikipiki ambao sasa ni moja ya
matatizo sugu yanayolalamikiwa na wateja wengi.Ukifunga kifaa cha
kudhibiti wizi katika pikipiki yako,hata kama ikiibiwa usiwe na
wasiwasi,itapatikana tu,”alisisitiza Kassam katika uzinduzi huo.
Salma
Rothbletz ni Mkuu wa Huduma kwa Wateja katika Kampuni hiyo,alisema
kifaa hicho maalum hufungwa katika pikipiki na kuunganishwa na simu ya
mkononi ambapo mteja hupata taarifa zote za uendeshaji wa pikipiki
katika siku yake.
Alifafanua
kuwa mfumo huo hudhibiti udanganyifu wa madereva katika matumizi ya
mafuta na umbali aliotumia kwa siku katika uendeshaji wa pikipiki,jambo
litakalowawezesha wamiliki wa pikipiki kuwa na uhakika wa mapato, kwa
zile zinazofanya usafiri wa abiria.
“Mfumo
huu utawasaidia wamiliki wa pikipiki za kusafirisha abiria kufuatilia
biashara yao kwa ukaribu na uhakika kwa kuwa wanaweza kujua kiasi cha
mafuta kilichotumika kwa siku na hata umbali ambao pikipiki imetembea,”
alifafanua.
Suhail
Sheriff ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya AfriTrack, amesema katika
uzinduzi huo kuwa mtandao huo wa udhibiti wa vyombo vya usafiri
unatumika pia katika malori na magari ya abiria na utasaidia kupunguza
ama kuondoa kabisa ajali za barabarani.
Amesema
kuwa mfumo huo hudhibiti hali ya dereva kama yuko timamu kuendesha
chombo husika na iwapo kuna dosari hutoa ishara ya tahadhari kwa dereva
mwenyewe na mwenye gari kabla ya madhara yoyote, ikiwa ni pamoja na
ajali, kutokea.
“Kama
gari lina hitilafu za kiufundi au dereva ana tatizo lolote, mathalan la
kiafya, mfumo hugundua na baada ya muda hutoa ishara ya tahadhari
unaosaidia hatua za kuzuia madhara yatokanayo na hitilafu hiyo
kuchukuliwa haraka,”alisema Mkurugenzi Mtendaji huyo.
Sheriff
amesema kuwa vyombo vya usafiri vinapokuwa katika maeneo yasiyo na
mtandao wa mawasiliano, ikiwa ni pamoja na porini na bahari kuu ambapo
mawasiliano ni magumu,wanatumia mfumo wa mawasiliano wa setelaiti
kufuatilia mwenendo wa vyombo hivyo katika maeneo hayo yasiyo na
mtandao.
Aidha
amesema kuwa mfumo huo tayari umeshaanza kwa mafanikio makubwa katika
nchi za Ivory Coast, Malawi,Zambia na sasa umeingia nchini katika miji
ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza na Mbeya
Kiure,
Omar Kiure ni Mwakilishi wa Kampuni ya Uhandisi ya amesema katika
uzinduzi huo kuwa mfumo huo wa udhibiri magari na madereva katika sekta
ya usafirishaji ni ukombozi kutokana na kukithiri kwa wizi hasa wa
mafuta unaosababisha hasara kubwa.
“Wizi
wa mafuta katika katika sekta ya usafirishaji na ujenzi ni sehemu ya
tatizo sugu na linalokera mno katika sekta ya ujenzi na kwa kweli mfumo
huu utatusaidia kudhibiti wizi huu unaotutia hasara mno na kusababisha
gharama kuwa juu,” alisema Kiure.
Athilyo
Choga ni Mwakilishi wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha amesema katika
uzunduzi huo kuwa mfumo huo wa udhibiti utasaidia jeshi hilo kudhibiti
na kupunguza au kumaliza kabisa tatizo la ajali za barabarani
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...