Na Mwandishi wetu

Dar es Salaam. Chama Cha Kuogelea Tanzania (TSA) kimezindua mafunzo ya mchezo wa kuogelea kwa shule za msingi na sekondari nchini.

Mafunzo hayo yenye lengo la kuutangaza mchezo huo na kuuendeleza, yatafanyika kwa shule sita za mkoa wa Dar es Salaam kwa kuanzia. Mafunzo hayo ni sehemu ya udhamini wa Shirikisho la kuogelea, Fina).

Mkurugenzi wa Ufundi wa TSA, Amina Mfaume alisema kuwa jumla ya wanafunzi 100 wamepata fursa ya kujifunza mafunzo hayo ambayo yanaendeshwa kwa njia ya kujitolea na makocha mbalimbali.

Mfaume alisema kuwa  wanafaunzi hao watapata fursa ya kuonyesha walichojifunza  Jumamosi (Oktoba 12) wkati wa maadhimisho ya Siku ya Kuogelea Duniani (Fina Aquatic day) kwenye bwawa la kuogelea la Shaaban Robert.

Alisema kuwa programu hiyo ina lengo la kuutangaza mchezo huo sambamba na kutafuta vipaji kwa ajili ya klabu na timu mbalimbali za Taifa na itaendeshwa nchi nzima kwa kipindi maalum.

“Tumeanza na shule sita, Diamond, Olympio na Upanga kwa shule za Msingi wakati na kwa upande wa sekondari ni Azania, Jangwani na Zanaki, baada ya shule hizo, makocha watatembelea shule mbalimbali ili kutafuta wanafunzi ambao watapata mafunzo zaidi, lengo ni kupata waogeleaji wengi zaidi wa vilabu na timu ya Taifa,” alisema Mfaume.

Alisema kuwa waogeleaji hao watapatiwa vifaa vya mchezo huo na kuviomba vilabu mbalimbali kufika siku ya kufunga ili kuchagua waogeleaji ambao watajiunga na timu zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...