Watuhumiwa wa wizi wa Mawe yenye dhahabu mali ya Mgodi wa North
Mara wakiwasili Mahakamani.
Watuhumiwa wa wizi wa dhahabu wakiwa katika Mahakama ya Hakimu
Mkazi wa Wilaya ya Tarime Mkoani Mara.
Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tarime.

*******************************

Na Tito Mselem Tarime,

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewafikisha
Mahakamani Watuhumiwa Wanane (8) kwa makosa mbalimbali
likiwemo la kuingia katika Mgodi wa North Mara na kuiba mifuko 15 ya
Mawe yenye Dhahabu yanayokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya
shilingi Milioni 234 za kitanzania.

Watuhumiwa hao waliingia Mgodini kwa nyakati tofauti kati ya tarehe 15
Septemba na 25 Septemba 2019 walikamatwa wakiwa na mawe mifuko
15 kinyume na Sheria.

Miongoni mwa watuhumiwa hao ni Zabron John (43), Jemes Makune
(35), Jonathan Chuwa (27), Amos Raphael (28), Mseti Chacha (29),
Chacha Marwa (29), Petro Mariba (32), na Samson Mathayo (17).

Akiwasomea mashtaka, Wakili wa Serikali Peter Ilole alitaja makosa yao
ni pamoja na kosa la kuhujumu uchumi, kutakatisha fedha, kuingia
mgodini bila kibali, kuiba mawe ya dhahabu pamoja na kukutwa na
madini bila kuwa na leseni ya uchimbaji au biashara ya madini.

Aidha, Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara Mohamed
Robert Silii, hakuwaruhusu watuhumiwa hao kujibu lolote kwa sababu
Mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza mashtaka yanayowakabili na
hivyo wakarudishwa rumande na kesi yao kuhairishwa hadi Oktoba 23,
2019 itakapotajwa tena.

Kosa la Kwanza ni kwa walishitakiwa wote Nane (8) kupanga njama
kinyume na sheria Wilayani Tarime Mkoa wa Mara na kuiba mawe ya
dhahabu katika mgodi wa Mgodi wa North Mara, kosa la Pili
watuhumiwa walikutwa wakiwa na mawe yenye madini bila ya kuwa na
leseni yoyote, Kosa la Tatu ni wizi wa mawe yenye dhahabu ambayo ni
mali ya Mgodi wa North Mara, Kosa la Nne ni utakatishaji wa fedha na
Kosa la Tano ni kuingia kwenye Mgodini bila ya kibali na kuiba mawe
yenye dhahabu yenye thamani ya shilingi 234,590,832/=.

Akizungumzia tukio hilo, Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo
amevipongeza Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kuwakamata
watuhumiwa hao na kutoa rai kwa watu wengine wenye tabia kama hizo
kuachana na wizi wa madini kwani Serkali iko macho kwa mtu yeyote
anayejihusisha na wizi wa madini.

Pia, Naibu Waziri Nyongo amevitaka Vyombo vya Ulinzi na Usalama
vihakikishe vinamkamata kiongozi wao Kitabo Ryoba Molel, ambaye
ndiye aliyedhamini wizi huo na baada ya kukamatwa alitoroka katika
kituo cha polisi Wilaya Tarime.

Ameongeza kitendo hicho cha kuwafikisha Mahakamani ni moja ya
jitihada zinazofanywa na Serikali katika kudhibiti wizi wa madini
unaojitokeza katika Migodi Mikubwa ambapo wafanyakazi wa Migodi
hiyo wanashirikiana na watu wa nje kuiba mali za wawekezaji.

Vilevile, Nyongo amewasisitiza wafanyabiashara wa madini kuyatumia
masoko ya madini kufanya biashara zao na kwa atakayebainika kufanya
biashara ya madini nje ya soko atakamatwa na kufikishwa Mahakamani
huku akiwaonya wale wote wanaokwepa kulipa kodi ya Serikali kuacha
mara moja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...