Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harisson Mwakyembe akizungumza leo wakazi wa Uzinduzi wa kipindi kipya cha michezo cha Sports Arena,sambamba na kuwatangaza watangazaji wapya wa kipindi hicho,hafla hiyo fupi umefanyika makao makuu ya ofisi za Wasafi Media,jijini Dar

Waziri Mwakyembe amempongeza Msanii mahiri wa muziki C.E.O wa Wasafi Media, Nassib Abdull almaarufu Diamond Platnumz kwa kuanzisha kipindi cha michezo na mchango wake mkubwa kuutangaza muziki nje ya mpaka wa Tanzania na kwingineko Duniani.

Akizungumza leo Jumatatu Oktoba 21,2019 kwenye uzinduzi wa kipindi hicho cha Sports Arena, Waziri Mwakyembe ameeleza kuwa taasisi ya Wasafi, imekuwa ikihamasisha hata wasanii wachanga kutaka kufikia mafanikio yake.“Nawashukuru sana Wasafi kwanza kwa kuweka hamasa kwenye muziki,Mtu yeyote anayeingia kwenye muziki sasa hivi anataka awe kama Diamond ni nzuri na hayo ndio maendeleo",ameeleza Dkt Mwakyembe.
C.E.O wa Wasafi Media, Nassib Abdull almaarufu Diamond Platnumz akizungumza jambo mbele ya wageni waalikwa kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harisson Mwakyembe kuzungumza na Wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo ikiwemo na kuzindua rasmi kipindi hicho,ambacho kilikuwa kikisubiriwa kwa hamu kubwa
C.E.O wa Wasafi Media, Nassib Abdull almaarufu Diamond Platnumz akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harisson Mwakyembe kuzungumza na Wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo ikiwemo na kuzindua rasmi kipindi hicho,ambacho kilikuwa kikisubiriwa kwa hamu kubwa .
Meneja wa Wasafi Media atambulikae kwa jina la Babu Tale akizungumza jambo huku akiwakaribisha wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo iliyowakutanisha wadau wa michezo,masumbwi,muziki na michezo mingine.
Mtangazaji mahiri atakaeongoza jahazi la kipindi cha Sports Arena Maulid Kitenga akizungumza jambo mara baaya kutambulishwa kwao na kipindi kuzinduliwa.
Kikosi kamilia cha kipindi cha Sports Arena ndani ya Wasafi Media
Ilikuwa ni burudani tuu na shangwe za hapa na pale
Watangazi nyota wa kpindi hicho kilichozinduliwa leo 
Baadhi wageni waalikwa na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua tukio la hafla hiyo.
Wageni waalikwa wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye hafla hiyo

Magari yaliyoandaliwa kwa ajili ya kuwabeba watangazaji wa kipindi hicho mara watakapokuwa wameshuka kwenye helikopta.
Helikopta iliyokuwa imewabeba Watangazaji mahiri wa kipindi cha Sports Arena ikiwa imetua uwanjani jirani na ofisi za Wasafi Media.




Wageni waalikwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...