Bei ya korosho kwa mnada wa pili umeongezeka na kufikia Sh. 2717/- kwa kilo moja ambapo mzigo wote uliopo tan 13,115 umeuzwa
Akitangaza Bei hiyo Meneja Mkuu wa TANECU Mohamed Mwinguku amesema kuwa korosho zilizopo kwenye maghala ya Chama Cha Ushirika Tandahimba na Newala (TANECU) zimenunuliwa zote
Amesema kuwa korosho kwa Wilaya ya Tandahimba imenunuliwa kwa sh 2717 kwa mnunuzi wa kwanza,wapili kanunua kwa sh 2697 na mnunuzi wa tatu amenunua kwa sh 2658
"Korosho iliyopo maghalani tayari tumeiuza yote kwa makampuni matatu Kati ya makampuni 37 yaliyojitokeza," amesema Mwanguku
Naye mkulima Hamis Hassan amesema pamoja na ongezeko Hilo malipo yafanyike kwa muda muafaka ili fedha zimfikie mkulima kwa wakati.
Katika mnada huo makampuni 37 na yalijitokeza,mnada mwingine wa tatu unatarajiwa kufanyika Wilaya ya Newala.
Meneja wa Chama Cha Ushirika Tandahimba na Newala (TANECU) Mohamed mwinguku akizungumza na w
Wadau wa zao la korosho wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...