Na Karama Kenyunko, globu ya jamii.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kesi ya Uhujumu Uchumi inayomkabili Mwandishi wa Habari za uchunguzi, Erick Kabendera hadi Novemba 20, mwaka huu kufuatia upande wa Mashtaka kudai upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Katika kesi hiyo, Kabendera anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji wa zaidi ya sh milioni 173.

Wakili wa serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amedai mbele ya Hakimu Mkazi, Vicky Mwaikambo kuwa Kesi hiyo leo Novemba 7, ilipangwa kwa ajili kutajwa, upelelezi wake bado haujakamilika pia Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizile aliyekuwa  akisikiliza kesi hiyo ameteuliwa kuwa jaji wa Mahakama Kuu hivyo ameiomba mahakama kuahirisha kesi hiyo wakati ikisubiri ipangiwe Hakimu mwingine wa kuendelea kuisikiliza.

Baada ya kusikiliza hoja hiyo, Hakimu Mwaikambo ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 20, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Katika shtaka la kwanza, Kabendera anadaiwa kujihusisha na mtandao wa kihalifu kwa kutoa msaada kwa genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia faida.

Pia anadaiwa kuwa bila ya sababu, alikwepa kodi ya Sh 173,247,047.02 ambayo ilitakiwa ilipwe kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Katika shtaka la tatu, kabendera anadaiwa kutakaisha Sh 173,247047.02 huku akijua fedha hizo ni mazalia ya kosa la kujihusisha na genge la uhalifu na utakatishaji fedha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...