Wanafunzi wakionyesha bango lenye ujumbe wa haki za watoto
mara baada ya kuzindua ajenda kuhusu haki za watoto uliofanyika kwenye Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.
Watoto kutoka Shule mbalimbali za Jijini Dar es Salaam, wakiwa katika
picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi, na viongozi wengine wa Serikali katika Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.
Watoto kutoka Kikundi cha Safi Theater cha Jijini Dar es Salaam,
wakionesha jinsi watoto wa shule wanavyofanyiwa ukatili wa kijinsia na
waendesha Bodaboda na Daladala na kukatishwa masomo, igizo lilitolewa katikaMaadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo chaMikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi (katikati),
akifurahia jambo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndungulile (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Ally Possi, mara baada ya kuwasili katika Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi, baada ya kuwasili katika Sherehe za Kuadhimisha ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere, leo Novemba 20, 2019, ambako alialikwa kuwa mgeni Rasmi.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi, akipata maelezo
kutoka kwa mtalaam kutoka Shirika la Watoto Duniani (UNICEF), katika moja ya banda lililokuwepo kwenye Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Dkt. Faustine Ndungulile, akizungumza na Washiriki wa Sherehe za
Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo chaMikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt.
Ally Possi, akizungumza na Washiriki wa Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.
Mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala mwaka wa
Tatu, Rose Mweleka, akiwasilisha mada kuhusu jinsi ya kutekeleza haki za watoto wa kike ikiwemo kuwafundisha hatua za makuzi ili kuwawezesha kukabiliana na hali wakifikia umri husika, Mada hiyo iliwasilishwa kwenye Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.

Picha na Idara ya Habari-MAELEZO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...