Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM) akiongozana na madiwani 11 wanawake wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga wamekutana na wanawake na mabinti wanaoishi katika kata ya Mwakitolyo ili kuzungumza nao namna ya kukomesha vitendo vya baadhi ya mabinti wenye umri kuanzia miaka 12 na wanawake watu wazima wanaofanya biashara ya kuuza miili yao maarufu ‘Chemsha chemsha’.

Hatua ya mbunge na madiwani hao kukutana na wanawake na mabinti wa Mwakitolyo leo Jumatatu Novemba 18,2019 inatokana na azimio la kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kilichofanyika Mwezi Agosti mwaka huu ambapo Mhe. Azza aliomba aongozane na madiwani wanawake kwa ajili ya kwenda kuzungumza na mabinti na akina mama ili kukomesha biashara ya ngono katika kata hiyo.

Akizungumza katika kikao cha ndani na wanawake hao wakiwemo wanaomiliki gesti na nyumba za kupanga kilichofanyika katika kijiji cha Nyaligongo,Mhe. Azza amesema biashara ya ngono inadhalilisha utu wa mwanamke lakini pia kuwaweka katika hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa mbalimbali ya zinaa hivyo inapaswa kupingwa na kila mtu.

“Ndugu zangu biashara ya ngono ni biashara ya kujidhalilisha naomba wanawake na mabinti wanaofanya biashara hiyo kuachana nayo. Tutafute kazi za kufanya ambazo siyo za kujidhalilisha,kazi yeyote ukiipenda na ukaifanya kwa moyo mmoja ni lazima utafikia malengo yako”,amesema Azza.

“Acheni biashara hii. Wanawake tutambue heshima tuliyopewa na mwenyezi Mungu,mama ndiyo anayejua kila kitu katika nyumba,mama ndiye aliyebeba majukumu makubwa katika familia,kwa hiyo tunatakiwa tuibebe heshima tuliyonayo badala ya kujidhalilisha”,alisema mbunge huyo.

Mhe. Azza ametumia fursa hiyo kuwataka wamiliki wa nyumba za kulala wageni ‘gesti’ na wanaopangisha vyumba kutoruhusu watu wanaofanya biashara ya kuuza miili.

Aidha amewashauri kuunda vikundi vya ujasiriamali na kuvisajili ili waweze kupata mikopo inayotolewa na halmashauri kwa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu na kwamba hata kama wana biashara zingine basi wajishughulishe pia na kilimo ili wawe na uhakika wa chakula katika familia zao.

“Nitumie fursa hii kumpongeza mtendaji wa kata ya Mwakitolyo na mashirika yasiyo ya kiserikali kwa kwenda kuwatafuta wanawake na mabinti waliokuwa wanafanya biashara na kuwapa elimu ya kuondokana na biashara hiyo na kuwapatia vyerehani ili waweze kufanya biashara ambayo ni halali,jambo ambalo limesaidia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa biashara hiyo”,ameongeza Azza. Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad(aliyefunga kitambaa cheupe katikati) akipokelewa na umati mkubwa wa wanawake akiwasili katika kata ya Mwakitolyo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga leo Jumatatu Novemba 18,2019. Picha zote na Said Nassor - Malunde 1 blog 
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad(aliyefunga kitambaa cheupe katikati) akipokelewa na umati mkubwa wa wanawake akiwasili katika kata ya Mwakitolyo.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad(aliyefunga kitambaa cheupe katikati) akipokelewa na umati mkubwa wa wanawake katika kata ya Mwakitolyo 
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akipokelewa katika kata ya Mwakitolyo. Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akizungumza na wanawake wa kata ya Mwakitolyo.

Wanawake wa Mwakitolyo wakimsikiliza Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akizungumza na wanawake wa kata ya Mwakitolyo.
Afisa Mtendaji wa kata ya Mwakitolyo Samson Lutonja akisoma taarifa ya kata ikiwemo biashara ya Chemsha chemsa
Mbunge wa Azza Hilal na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga wakisikiliza taarifa ya kata ya Mwakitolyo.
Diwani wa kata ya Mwakitolyo Limbe Augustine Limbe akizungumza katika kikao hicho.
Akina mama wakiwa kwenye kikao hicho.
Diwani wa viti maalumu Chausiku Hassan akizungumza katika kikao hicho. 
Wanakikundi wakisoma risala mbele ya Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad 
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akimkabidhi Afisa Mtendaji wa kata ya Mwakitolyo Samson Lutonja Eploni 50 kwa ajili ya Mama Lishe katika kata ya Mwakitolyo.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akizungumza na baadhi ya mama lishe baada ya kuwakabidhi Eploni nyekundu zitakazowasaidia kwenye kazi yao.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akizungumza na baadhi ya mama lishe waliohudhuria kikao cha ndani cha mbunge,madiwani wanawake wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akipiga picha ya pamoja na Mama lishe pamoja viongozi wa halmashauri na kata.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akipiga picha ya pamoja na viongozi wa chama cha wachimbaji wadogo wanawake kata ya Mwakitolyo.Chama hicho kimemuomba Mbunge kuwa Mlezi wa chama hicho.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akipiga picha ya pamoja viongozi wa kikundi cha hiari ya Moyo kijiji cha Nyaligongo kata ya Mwakitolyo kinachojihusisha na kuweka na kukopa.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akipiga picha ya pamoja viongozi wa kikundi cha hiari ya Moyo kijiji cha Nyaligongo kata ya Mwakitolyo.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akipiga picha na kikundi cha wanawake na maendeleo kilichoanzishwa kwa lengo la kuwafanya akina mama kuachana na biashara ya kuuza miili yao.Dhamira ya kikundi hicho ni kushusha Punda 200 'ndoo za mawe ya dhahabu' ili kusafisha senga 'mchanga wa dhahabu" 
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akiagana na akina mama wa Mwakitolyo.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga,Mhe. Azza Hilal Hamad akiagana na akina mama wa Mwakitolyo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...