Na Karama Kenyunko, Michuzi Globu ya jamii 

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu Naibu Mkurugenzi Mazingira na Afya kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Elias Chinàmo kulipa faini ya Sh. milioni 7 au kutumikia kifungo cha miaka 3 gerezani baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka 14 ya kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Pia Hakimu Mkazi , Augustina Mmbando aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, amemuamuru mshtakiwa huyo kulipà jumla ya sh milioni 18 ambazo anadaiwa kuchukua wakati wa utendaji wa makosa hayo.

Katika kesi hiyo, Chinamo alikuwa akikabiliwa na jumla ya mashtaka 28,14 ya kujihusisha na vitendo vya rushwa na 14 ya wizi àkiwa mtumishi.

Alitiwa hatiani katika mashtaka 14 ya kujihusisha na vitendo vya rushwa ambapo mahakama ilimuhukumu kulipa fàini ya sh.500,000 kila kosa au kwenda jela miaka 3 kilakosa.Upande wa mashtaka uliokuwa ukiwakilishwa na wakili wa serikali kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupàmbana na Rushwa Leonard Swai ,ulikuwa na jumla ya mashahidi wanane na vielelezo sita.

Hata hivyo, mshtàkiwa huyo amefànikiwa kulipà faini ya sh milioni 7 huku sh milioni 18 àmeamuliwa kuzilipa ndani ya mwaka mmoja.

Katika kesi hiyo ilidaiwa kuwa, katika nyakati tofauti kati ya mwaka 20011 na 2012 jijini Dar es Salaam,katika benki ya CRDB tawi la Holland na NBC tawi la Kichwele alijipatia jumla ya Sh milioni 18 kwa manufaa yake binafsi kupitia akanti zake zilizo katika matawi ya benki hizo.

Ilidaiwa alijipatia fedha hizo kutoka kwa watu mbalimbali akiwemo Anyitike Kitalima, Joseph Bilago, Emanuela Safari ,Fadhili Kinemile ,Suzana Mchala kiwango ambacho kama manufaa kwake ili aweze kuwapa nafasi nyingine ya kuratibu semina na warsha mbalimbali jambo ambalo lilikuwa chini ya mamlaka ya mwajiri wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...