Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Faustina Mfinanga Maarufu kama Nandy anayetamba na wimbo wake mpya wa Magufuli amepishana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Nandy aliyetakiwa kutumbuiza leo katika ufunguzi wa Mkutano wa mawaziri wa Mambo ya Nje 34 wa nchi za Afrika 29 na nchi tano za Nordic ameshindwa kufanya hivyo baada ya kuchelewa kufika na kutokuruhusiwa kuingia ndani.

Taarifa zinasema, Nandy alitakuwa kuwasili mapema saa 2 asubuhi kabla Rais hajafika ila alijikuta anafika saa 3 na tayari ufunguzi wa Mkutano huo ukiwa umeanza.

Kutokana na tukio hilo, nenda ambaye alikua ni msanii.pekee aliyetakiwa kutumbuiza kwenye ufunguzi huo ameshindwa baada ya kushindwa kufika kwa muda aliopangiwa.

Nandy amekuwa ni miongoni mwa wasanii waliopata fursa ya kutumbuiza katika mikutano mikumbwa mbalimbali na kibao chake kipya kiitwacho Magufuli

Rais Dkt Magufuli amefungua mkutano wa mawaziri wa Mambo ya Nje 34 wa nchi za Afrika 29 na nchi tano za Nordic ambao umeanza Novemba 8 mwaka huu nchini Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...