Msichana Rose Manumba Chini ya Umri wa Miaka 30, ameingia Katika Orodha ya Wajumbe wa kushauri Taasisi ya Umoja wa Mataifa wa Wanawake Tanzania (UN Women Tanzania) 2019 - 2021
Rose Manumba ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania, amechaguliwa kuwa miongoni mwa wajumbe wanaotokana na Asasi za Kiraia kuingia katika kikundi cha kushauri (Civil Society Advisory Group) Umoja wa Mataifa wa Wanawake Tanzania (UN Women Tanzania) namna gani tunaweza kufikia moja ya malengo ya maendeleo endelevu hususani lengo la 5 la Usawa wa Kijinsia (Gender Equality) katika maeneo mbalimbali.
Kikundi hicho cha washauri kina jumla ya Idadi ya Wajumbe wasiozidi 10 wanaotokea kwenye Taasisi mbalimbali.
Kikao cha kwanza kimefanyika jana Novemba 20/2019 na kufunguliwa rasmi na Naibu Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake Tanzania (Deputy Country Representative to UN Women Tanzania) Bi. Julie Taylor.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...