Msichana Rose Manumba Chini ya Umri wa Miaka 30,  ameingia Katika Orodha ya Wajumbe wa kushauri Taasisi ya Umoja wa Mataifa wa Wanawake Tanzania (UN Women Tanzania) 2019 - 2021 

 Rose Manumba ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania, amechaguliwa kuwa miongoni mwa wajumbe wanaotokana na Asasi za Kiraia kuingia katika kikundi cha kushauri (Civil Society Advisory Group) Umoja wa Mataifa wa Wanawake Tanzania (UN Women Tanzania) namna gani tunaweza kufikia moja ya malengo ya maendeleo endelevu hususani lengo la 5 la Usawa wa Kijinsia (Gender Equality) katika maeneo mbalimbali.

Kikundi hicho cha washauri kina jumla ya Idadi ya Wajumbe wasiozidi 10 wanaotokea kwenye Taasisi mbalimbali.

Kikao cha kwanza kimefanyika  jana  Novemba 20/2019  na kufunguliwa rasmi na Naibu Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake Tanzania (Deputy Country Representative to UN Women Tanzania) Bi. Julie Taylor.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...