Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (katikati) katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Wabunge, Viongozi mbali mbali wa kiserikali na Viongozi kutoka asasi mbali mbali zisizo za kiserikali baada ya kufunga maonesho ya wiki ya asasi zisizo za kiserikali 2019, kushiriki dhifa ya pamoja na ugawaji wa tuzo kwa asasi zilizofanya vizuri leo katika hoteli ya Morena Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na wafanyakazi wa asasi zisizo za kiserikali wakati akifunga maonesho ya wiki ya asasi zisizo za kiserikali 2019, kushiriki dhifa ya pamoja na ugawaji wa tuzo kwa asasi zilizofanya vizuri leo katika hoteli ya Morena Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia) akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Wajibu, Ndg. Ludovick Utouh kwa ajili ya kufunga maonesho ya wiki ya asasi zisizo za kiserikali 2019, kushiriki dhifa ya pamoja na ugawaji wa tuzo kwa asasi zilizofanya vizuri tukio lililofanyika leo katika hoteli ya Morena Jijini Dodoma. Kuanzia kushoto ni Rais wa asasi zisizo za kiserikali, Ndg. Stigma Tenga na Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Pamela O’Donnell.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akipokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Wajibu, Ndg. Ludovick Utouh alipowasili kwa ajili ya kufunga maonesho ya wiki ya asasi zisizo za kiserikali 2019, kushiriki dhifa ya pamoja na ugawaji wa tuzo kwa asasi zilizofanya vizuri tukio lililofanyika leo katika hoteli ya Morena Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akigawa tuzo ya Mshindi wa Jumla kutoka Femina, iliyopokelewa na Mkurugenzi wa Habari wa Shirika hilo, Ndg. Amabili Batamula, kwa asasi zisizo za kiserikali wakati akifunga maonesho ya wiki ya asasi zisizo za kiserikali 2019, leo katika hoteli ya Morena Jijini Dodoma. Kushoto ni Balozi wa Canada nchini Tanzania, Mhe. Pamela O’Donnell na kulia ni Rais wa asasi zisizo za kiserikali , Ndg. Stigma Tenga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...