Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Mchezo wa kwanza wa kufuzu michuano ya mataifa Afrika AFCON 2021 kati ya Tanzania na Equatorial Guinea umemalizika kwa Taifa Stars kuibuka na ushindi wa bao 2-1.

Taifa Stars leo imeanza vema michuano ya Afcon kwa kuibuka kidedea mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa.

Stars ilianza kwa kasi kipindi cha kwanza lakini ilishindwa kuweza kutumia nafasi walizozipata na katika dakika ya 15 Equatorial Guinea aliweza kupata bao la kwanza kupitia kwa mchezaji wake Pedro Obiang.

Kipindi cha pili Stars ilianza kwa kulazimisha mashambulizi na iliwapeleka mpaka dakika ya 68 ambapo Simon Msuva aliandika bao la kwanza akimalizia pasi ya Mohamed Hussein 'Tshabalala' na kuweka mzani sawa.

Taifa Stars iliendelea kushambulia ikitafuta goli la ushindi na kupitia kwa Kiungo Salum Abubakari kwenye dakika ya 90 aliandika bao la lipi na la ushindi akiwa nje ya 18.

Ushindi huo unaifanya Stars kujikusanyia pointi zake tatu leo ikiwa kwenye uwanja wa Taifa na Novemba 20, Taifa Stars watashuka tena kucheza na Libya ukiwa ni mchezo wa pili.

Kikosi cha timu ya Taifa Stars
Equatorial Guinea








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...