Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza mbele ya Viongozi wa dini katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam leo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akisalimiana na baadhi ya viongozi wa dini hapa nchini katika Mkutano uliowahusisha viongozi hao pamoja na Mkuu wa Mkoa huyu katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam leo.
Viongozi wa Dini Mbalimbali hapa nchini wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh.Paul Makonda katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam leo.

**********************************

Viongozi wa Dini wakiwemo Maaskofu, Mashekhe, Wachungaji,Manabii, Maimamu na Wainjilisti Mkoa wa Dar es salaam leo November 18 wametoka na azimio la pamoja la kumuunga Mkono Rais Dkt. John Magufuli katika jitiada zake za kuleta maendeleo kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali inayolenga kumaliza kero za Wananchi.

Hatua ya Viongozi hao wa dini imekuja baada ya Kuvutiwa na taarifa iliyowasilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda dhidi ya Miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa kwenye Mkoa huo chini uongozi thabiti wa Rais Dkt. John Magufuli jambo lililowakosha Viongozi wa Dini na Kuamua kuja na tamko hilo.

Katika mkutano huo RC Makonda amewasilisha kwa Uhalisia wa Video taarifa ya miradi iliyotekelezwa na serikali katika sekta zote muhimu ikiwemo Afya, Barabara, Maji, Umeme, Elimu, Viwanda, Usafirishaji na sekta anyinginezo jambo lilikowagusa viongozi wa dini.

Pamoja na hayo Viongozi hao wa Dini wamesema wataendelea kumuombea Rais Dkt. John Magufuli azidi kuwa na Nguvu na uwezo wa kuwatumikia wananchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...