.Mh Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu(kulia) pamoja na Mkuu wa
Wilaya Ya Kilosa Mh Adamu Mgoyi (mwenye shati ya draft )na baadhi ya
wananchi wa kijiji hicho wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa umeme wa rea katika awamu ya tatu mzunguko wa kwanza katika kijiji cha mabana kata ya mbigiri wilaya ya kilosa mkoani morogoro hapo jana .
Mh Naibu Waziri wa nishati Subira Mgalu pamoja na Mkuu Wa Wilaya ya
Kilosa Mh Adamu Mgoyi na baadhi ya wananchi wa kijiji cha mabana kata ya mbigiri wakizungumza na wananchi kabla ya kukata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa umeme wa rea katika awamu ya tatu mzunguko wa kwanza wilayani kilosa mkoani morogoro 
Mkuu Wa Wilaya Ya Kilosa Mh Adam Mgoi (Aliesimama) Akizungumza Na
Wananchi Wa Kata Ya Mvuha Ndani Ya Wilaya Hiyo Baada Ya Ugeni Wa Naibu Waziri wa Nishati Mh Subira Mgalu Kutembelea Wilaya Hiyo.
Baadhi Ya Wananchi Wa Kijiji Cha Makwambe Kata Ya Mvumi Wilayani
Kilosa Wakimskiliza Naibu Waziri Wa Nishati Bi Subira Mgalu Alipotembelea Kijiji Hicho.

*********************************

NA FARIDA SAIDY,MOROGORO.

Wakandarasi Wa Mradi Wa Rea Katika Awamu Ya Tatu Mzunguko Wa Kwanza Wametakiwa Kutekeleza Majukumu Yao Kikamilifu Ili Kufanikisha Adhma Ya Serikali Ya Kuwaletea Wananchi Maendeleo Katika Maeneo Yao Ikiwa Uunganishwaji Wa Umeme Huo Katika Vijiji Utaleta Manufaa Makubwa Ikiwemo Uuanzishwaji Wa Viwanda Vidogo Vidogo Kuelekea Uchumi Wa Kati.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Naibu Waziri Wa Nishati Bi Subira Mgalu
Alipotembelea Katika Kijiji Cha Mabana Kata Ya Mbigiri Wilayani Kilosa
Mkoani Morogoro Kwa Ajili Ya Uzinduzi wa Uwashaji Wa Umeme, Na kuongea na wananchi wa kijiji Makwambe Kata Ya Mvumi Wanaotarajiwa Kupatiwa Umeme Kupitia Mradi Huo.

Mh.Mgalu Amesema Kumekuwa Na Malamiko Mengi Kutoka Kwa Wananchi
Hasa Kuhusu Michoro Inayoidhinishwa Na Bodi Katika Uwekaji Wa Nguzo Za Umeme Hivyo Limekwisha Tatuliwa Tatizo Hilo Na Kama Wizara Wametoa Maelekezo Ya Namna Ya Michoro Hiyo Kama Ilivyoidhinishwa Na Bodi Ya Wakala Wa Vijijini Rea.

Kwa Upande Wake Kaimu Meneja Tanesco Bw.Martin Schilima Na Mkuu Wa
Wilaya Ya Kilosa Mh Adam Mgoi Wameishukuru Serikali Kupitia Naibu Waziri Mh Subira Mgalu Kwa Hatua Na Jitihada Zinazofanyika Katika Kuwafikia Wananchi Kwa Kuwaunganishia Umeme Na Kuahidi Kushirikiano Nao Pamoja Na Wananchi Kwa Kila Hatua Ili Kuwafikia Kwa Wakati.

Nao Baadhi Ya Wananchi Wa Kijiji Cha Mabana Kata Ya Mbigiri Wametoa
Shukrani Zao Kwa Kuwashiwa Umeme Katika Kijiji Hicho Na Kuahidi Kufanya Makubwa Katika Kuwaletea Maendeleo Hasa Uanzishwaji Wa Viwanda Vidogo Vidogo Kama Kusindika Nyanya.

Mradi Huu Upo Katika Awamu Ya Tatu Mzunguko Wa Kwanza Ambapo Kuna
Vijiji Mia Moja Na Sitini Na Tano Katika Mkoa Wa Morogoro Ambapo Katika
Wilaya Ya Kilosa Kuna Vijiji 24 Na Mpaka Sasa Vijiji Kumi Vimeshawashwa
Umeme Na Vijiji Vilivyosalia Kumi Na 4 Vinakwenda Kuwashwa Umeme Kabla Ya Mwezi Desember Mwaka Huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...