Baadhi ya wakazi
wa mtaa wa Yespa Manispaa ya Morogoro wakiwa nje ya nyumba zilizozingirwa na
maji.
……………………………..
NA FARIDA SAIDY,
MOROGORO
Baadhi ya kaya zilizo
kandokando ya Mto Ngerengere Mtaa wa Yespa Manispaa ya Morogoro zimezingirwa na
maji na kusababisha wakazi wa mtaa huu kuhama
kwa muda, ambapo imeelezwa hali hiyo imesababishwa na Maji kupoteza
mwelekeo baada ya sehemu ya mto kuzibwa katika ujenzi wa Reli ya kisasa.
Wakiongea kwa nyakati
tofauti wakazi hao wamesema kuwa hali hiyo imesababishwa na maji kupoteza
mwelekeo kufuatia ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa ambao imesababisha
maji kujaa katika makazi ya watu.
Aidha wakazi hao wamesema
kuwa hali hiyo ya maji kuingia kwenye maeneo
ya makazi imetajwa kusababisha hasara, ambapo licha ya baadhi ya watu
kulazimika kuyahama makazi yao kwa muda, pia baadhi ya huduma zimesimama
ikiwemo ibada.
Wakazi hawa walio
pembezoni mwa mto Ngerengere wamesema kuwa wengi wao wameishi kwa muda mrefu katika
maeneo hayo lakini wajawahi kukutana na changamoto
ya kuzingirwa na maji hivyo swala hilo kwao wanaliona ni tatizo hivyo wanaiomba
mamlaka husika kulichulia hatua.
Pamoja na kaya zilizo
zingirwa na maji kuwa pembezoni mwa mto Ngerengere, Malalamiko ya wakazi hao ni
ujenzi wa Reli ya kisasa, wakidai sehemu kubwa ya mto imezibwa ambapo kufuatia
mvua zinazo endelea kunyesha mto huo umefurika na maji kusambaa baada ya kukosa
mwelekeo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...