Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Kutokana na tamaduni za nchi ya Saudi Arabia, Pambano la ngumi kati ya Antony Joshua na  Andy Ruiz Jr hakutakuwa  wasichana (Boxing Ring Girls) wanaopita kuonyesha raundi kila linapotaka kuanza.

Pambano hilo litakalofanyika Jumamosi usiku Disemba 7,  kwa mara ya kwanza hakutakuwa na wale wasichana wanaopita kuonyesha raundi kila inapotaka kuanza.

Uamuzi huo umechukuliwa kutokana na kuheshimu utamaduni wa Saudi Arabia, ambao sheria zao zinakataza wanawake kujitokeza hadharani wakiwa na mavazi yanayoonyesha mwili wao.

Joshua atakuwa na hamu kubwa ya kupata ushindi jijini Diriyah baada ya Ruiz kushangaza ulimwengu wa ngumi Juni mwaka huu kwa kumchapa Muingereza huyo katika raundi ya saba kwenye Ukumbi wa Madison Square Garden.

Mwanzoni ilikuwa inaonekana Joshua na Ruiz wangepigania Cardiff kabla ya Saudi Arabia kunyakuwa pambano hilo. Joshua, tayari amewasili Saudia kwa lengo la kumalizia mazoezi yake ya mwisho kuelekea katika pambano hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...