Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi. Dorothy Mwaluko akimueleza Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella,   juu ya umuhimu wa kukamilisha  kwa wakati  shughuli zitakazo fanyika siku ya sherehe za maadhimisho ya  miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri zitakayofanyika mkoani Mwanza katika viwanja vya CCM Kirumba, wakati alipofika uwanjani hapo kukagua maandalizi ya sherehe hizo leo, tarehe 5 Desemba, 2019.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi. Dorothy Mwaluko na Mkuu mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella (kushoto) pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa huo, Christopher Kadio, leo, tarehe 5 Desemba, 2019,  wakiwa katika viwanja vya CCM Kirumba, wakati alipofika uwanjani hapo kukagua maandalizi ya sherehe za maadhimisho ya  miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri zitakayofanyika mkoani humo
Kikundi cha Kwaya cha MVC kikifanya  mazoezi kwa ajili ya siku ya sherehe za maadhimisho ya  miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri zitakayofanyika mkoani Mwanza katika viwanja vya CCM Kirumba tarehe 9 Desemba 2019. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya Jamhuri; Uzalendo, Uwajibikaji na Ubunifu ni msingi wa Ujenzi wa Uchumi wa Taifa letu”.
Mkuu wa majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo,   leo, tarehe 5 Desemba, 2019 akishuka  katika jukwaa la Uwanja wa CCM  Kirumba, mkoani Mwanza mara baada ya kukagua shughuli za maandalizi za  Majeshi ya Ulinzi kwa ajili ya   siku ya sherehe za maadhimisho ya  miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri zitakayofanyika mkoani humo tarehe 9 Desemba 2019. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya Jamhuri; Uzalendo, Uwajibikaji na Ubunifu ni msingi wa Ujenzi wa Uchumi wa Taifa letu”.
Mkuu wa majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo, akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella,  leo, tarehe 5 Desemba, baada ya kukagua shughuli za maandalizi za  Majeshi ya Ulinzi kwa ajili ya   siku ya sherehe za maadhimisho ya  miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri zitakayofanyika mkoani humo tarehe 9 Desemba 2019, katika viwanja vya CCM Kirumba. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya Jamhuri; Uzalendo, Uwajibikaji na Ubunifu ni msingi wa Ujenzi wa Uchumi wa Taifa letu”.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...