Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu
(Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi. Dorothy Mwaluko akimueleza Mkuu wa mkoa
wa Mwanza Mhe. John Mongella, juu ya umuhimu wa kukamilisha kwa
wakati shughuli zitakazo fanyika siku ya sherehe za maadhimisho ya
miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri zitakayofanyika mkoani Mwanza
katika viwanja vya CCM Kirumba, wakati alipofika uwanjani hapo kukagua
maandalizi ya sherehe hizo leo, tarehe 5 Desemba, 2019.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu
(Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi. Dorothy Mwaluko na Mkuu mkoa wa Mwanza
Mhe. John Mongella (kushoto) pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa huo,
Christopher Kadio, leo, tarehe 5 Desemba, 2019, wakiwa katika viwanja
vya CCM Kirumba, wakati alipofika uwanjani hapo kukagua maandalizi
ya sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri
zitakayofanyika mkoani humo
Kikundi cha Kwaya cha MVC
kikifanya mazoezi kwa ajili ya siku ya sherehe za maadhimisho ya miaka
58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri zitakayofanyika mkoani Mwanza katika
viwanja vya CCM Kirumba tarehe 9 Desemba 2019. Kauli mbiu ya mwaka huu
ni “Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya Jamhuri; Uzalendo, Uwajibikaji na
Ubunifu ni msingi wa Ujenzi wa Uchumi wa Taifa letu”.
Mkuu wa majeshi
ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo, leo, tarehe 5 Desemba, 2019
akishuka katika jukwaa la Uwanja wa CCM Kirumba, mkoani Mwanza mara
baada ya kukagua shughuli za maandalizi za Majeshi ya Ulinzi kwa ajili
ya siku ya sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya
Jamhuri zitakayofanyika mkoani humo tarehe 9 Desemba 2019. Kauli mbiu
ya mwaka huu ni “Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya Jamhuri; Uzalendo,
Uwajibikaji na Ubunifu ni msingi wa Ujenzi wa Uchumi wa Taifa letu”.
Mkuu wa majeshi
ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo, akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa
Mwanza Mhe. John Mongella, leo, tarehe 5 Desemba, baada ya kukagua
shughuli za maandalizi za Majeshi ya Ulinzi kwa ajili ya siku ya
sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri
zitakayofanyika mkoani humo tarehe 9 Desemba 2019, katika viwanja vya
CCM Kirumba. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57
ya Jamhuri; Uzalendo, Uwajibikaji na Ubunifu ni msingi wa Ujenzi wa
Uchumi wa Taifa letu”.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...