Shindano la Urembo Dunia Miss World 2019, limefanyika usiku wa kuamkia Desemba 15, na Mrembo kutoka nchi ya Jamaica Toni-Ann Singh ametwaa taji hilo.

Toni-Ann ameitoa kimasomaso nchi yake mara baada ya kutwaa taji la Urembo wa Dunia katika mashindano ya kumsaka mlimbwende wa Dunia (Miss World), yaliyofanyika Jijini London, nchini Uingereza.

Shindano hilo ambalo jana ilikuwa ni mara yake ya 69 kufanyika, lilikutanisha warembo kutoka Mataifa mbalimbali duniani, ambapo nchi ya Tanzania iliwakilishwa na Mrembo Sylvia Sebastian Bebwa, ambaye yeye kwa juma lililopita aliingia katika 20 bora ya warembo wenye vipaji, baada ya yeye kuonesha kipaji cha kucheza 'Robot Dance'.

Mbali na Urembo, Mlimbwende huyo wa Dunia anapenda kutoa Elimu ya afya ya akili na matarajio yake ni kuwa Daktari na taji lake amelipokea kutoka kwa Venessa Ponce De Leon, Mrembo kutoka nchini Mexico alitwaa taji hilo mwaka 2018.

Katika mashindano hayo mshindi wa pili alikuwa mrembo kutoka Ufaransa, Ophely Mezino, wa tatu ni Suman Rao kutokea nchini India


Warembo waliofanikiwa kuingia 12 bora ya  Miss World 2019 Top
Kenya, Nigeria , Brazil ,Mexico ,India ,Nepal ,Philippines , Vietnam ,Jamaica, France ,Russia  na Cook Islands
 Miss World 2019 Toni-Ann Singh akiwa na wazazi wake baada ya kutwaa taji la urembo
Miss World 2019 Toni-Ann Singh akiwa katikati ya mshindi wa Pili Kutoka Ufaransa Ophley Mezino (Kushoto) na Sumao Rao kutoka India
 Kumi 10 ya Miss World 2019


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...