Taasisi ya Ustawi wa Jamii imenyakua nafasi ya kwanza na kupata tuzo ya umahiri katika uandaaji wa Taarifa za Fedha ya Mwaka 2018 (Best Presented Financial Statements for the Year 2018 Awards) inayotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) katika hafla iliyofanyika Disemba 7, jioni katika viwanja vya NBAA Bunju.
Kwa mara ya nne mfululizo Taasisi ya Ustawi wa Jamii inashiriki na Kunyakua ushindi kwenye tuzo hizi muhimu katika taaluma ya Uhasibu Tanzania.
Akiongea baada ya Kupokea tuzo Mkuu wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce Nyoni amesema ni furaha kubwa kwa Taasisi kutunukiwa tuzo hii ambayo ni kielelezo cha weledi na umahiri wa hali ya juu wa utunzaji wa taarifa za fedha na menejimenti nzuri za fedha za serikali katika Taasisi Yetu.
"Tumekuwa tukitoa huduma ya taaluma ya elimu, na ni manguli wa kutoa na kufundisha katika taaluma ya ustawi wa Jamii lakini sasa tunaonyesha weledi mkubwa katika fani ya uhasibu na utunzaji taarifa za fedha, naipongeza sana timu yangu ya Uhasibu ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii ikiongozwa na CPA Athuman Senzota." alisema Dkt. Joyce.
Mkuu
wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce Nyoni akipokea Tuzo ya Mshindi
wa Kwazna ya uandaaji taarifa za fedha kwa mwaka 2018 katika kundi la
Vyuo vya elimu ya Juu,
Kutoka
Kushoto Dkt. Joyce Nyoni Mkuu wa Taasisi, Dkt. Zena Mabeyo Kaimu mkuu
wa Taasisi fedhaUtawala, CPA Aisha Kapande Mhasibu,CPA Manase Shunashu
Mhasibu, Na nyuma CPA Athman senzota Mhasibu Mkuu
Mkuu wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii na timu yake wakifurahia ushindi wa Tuzo ya kwazna ya Uandaaji wa taarifa za fedha 2018
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...