Moja ya barabara ambayo bado haijazibwa viraka.
Mchoro kwaajili ya maandalizi ya kuziba sehemu ya barabara iliyoharibika
Muonekano wa barabara iliyozibwa kwa kutumia lami ya baridi  baada ya kuzibwa viraka maeneo yaliyoharibika.

Na Irene Mwidima, Globu ya jamii
TANGU kuzinduliwa kwa teknolojia mpya ya uzalishaji wa lami hapa nchini Oktoba, 2014 bado kumekuwa na changamoto ya kutokupangiwa matumizi ya kujenga barabara na Serikali.

Hayo yamesemwa na Meneja masoko wa kampuni ya Starpeco LimitedJones Mkoka wakati akizungumza na michuzi blog leo katika maonesho ya nne ya bidhaa za viwanda yanayofanyika jijini Dar es Salaam.

Makoka amesema teknolojia hiyo ni rahisi kwani huchnganywa na maji ya baridi na kufanya kazi kama lami inayochemshwa

"Ujenzi wa barabara zote upo chini ya TANROAD na TARURA,  na wao ndio hutoa tenda za ukandarasi wa barabara, huwa wanatoa aina na viwango vinavyotakiwa na mradi husika,  lami yetu bado haijaanza kuruhusiwa kwenye ujenzi wa barabara". Amesema Mkoka

Licha Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kushirikiana na chuo kikuu cha Dar es Salaam katika kutatua changamoto mbalimbali katika jamii bado wabunifu wa lami hiyo hawajapata tenda ya kutengeneza hata barabara moja.

Licha ya kuwa na chngamoto hiyo kampuni ya kampuni ya Starpeco Limited imeweza kuuweka viraka katika barabara ya Changanyikeni na barabara ya uvumbuzi zilizopo chuo kikuu cha Dar es Salaam, pamoja na kumwaga lami mpya katika baraara ya Kileleni yenye urefu wa Kilomita 120.

Aidha amesema kuwa baada ya kuona changamoto hiyo wakona wajitokeze mbele waweze kueleza jinsi inavyoweza kutumika kwa urahisi lami hiyo ya baridi kutengenezea barabara.

"kwahiyo baada ya kuona changamoto hiyo tukaona ni bora tujitokeze mbele tuweze kueleza jinsi inavyoweza kutumika,  na tunashukuru wazo letu liliweza kupokelewa na kazi tumeanza,  tumeweza kuirekebisha barabara ya Kileleni, lakini pia tuliweza kuziba viraka vya barabara ya Uvumbuzi kutoka kutoka maeneo ya Utawala mpaka chuo cha COET".

Kiwanda cha lami baridi inayochanganywa na maji kipo Kipawa jijini Dar es salaam na kilianzishwa mwaka 2014,  na faida kubwa ya hii lami inaruhu ujenzi wa barabara bila kuchemaha lami,  kama ijulikanavyo lami zingine za kawaida ni lazima zichemshwe kwa ajili ya kuchanganywa na kokoto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...