Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (wa pili toka kulia) akiwa pamoja na wakulima katika kijiji cha Kalalasi kata ya Mkali wilayani Kalambo akiwa pamoja na wakulima wa kijiji hicho wakisaidiana kusukuma plau ikiwa moja ya njia ya kuhamasisha kilimo katika maeneo ya vijijini.

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Julieth Binyura akisaidiana na mmoja wa wakulima wa kijiji cha Kalalasi Kata ya Mkali Wilayani Kalambo ikiwa ni moja ya kuhamasisha kilimo katika msimu huu wa kilimo wa mwaka 2019/2010 katika mkoa wa Rukwa.



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akielekeza namna ya kupanda mahindi kwa kufuta vipimo vinavyoelekezwa na wataalamu wa kilimo na hatumae kufanya kilimo cha Tija.

………………………………………………

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wakulima wa Mkoa huo kuhakikisha wanafuata maelekezo ya maafisa kilimo waliopo kwenye ngazi za vijiji na kata ili kuweza kulima kwa tija na hatimae kuongeza upatikanaji wa chakula katika mkoa na pia kujiongezea kipato.

Amesema kuwa ni dhamira ya mkoa kuhamasisha kilimo kinachoongeza uzalishaji kwa ekari moja, hivyo ni lazima wakulima wapande kwa kutumia utaalamu huku wakizingatia ubora wa mbegu ambazo zimehakikiwa na Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu nchini (TOSC) pamoja na kutumia mbolea zinazostahili kwa ekari kama ambavyo wataalamu wanashauri

“Sio mtu anachukua mfuko mmoja wa mbolea halafu anakwenda kuuweka katika ekari mbili matokeo yake uzalishaji unakuwa ni mdogo, lakini pia baada ya mahindi kuwa yameota na kuwekewa mbolea ni lazima pia kuangalia upande wa visumbufu, wadudu wale waharibifu wa mazao, lazima tuweke dawa mapema tutumie viuatilifu ambavyo vinashauriwa na wataalamu wa kilimo, baada ya hpo tuangalie mashamba yetu kwa kupalilia kwa kufanya hivi tunaweza kuzidfi hata gunia 20 kwa ekari,” Alisema.

Ameyasema hayo alipokuwa katika ziara yake maalum ya kuhamasisha kilimo chenye tija katika Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Mkoani humo akiwa pamoja na wataalamu wa kilimo wa mkoa na halmashauri pamoja na mkuu wa Wilaya hiyo.

Kwa upande wao mmoja wa wamiliki wa shamba lililotembelewa na Mkuu wa Mkoa Bwana Rojas Lukas amesema kuwa changamoto ubwa inayowakuta wakulima na kushindwa kuendelea kulima kilimo chenye tija ni mitaji pamoja na mdudu mharibifu aina ya kiwavi jeshi.

“Kuna mdudu Fulani anaitwa Kiwavi jeshi Yule anatusumbua sananingeomba serikali ijaribu kututafutia dawa ambayo inaweza ikamuua Yule mdudu, kingine tunaomba serikali itusaidie kama inawezekana watukopeshe ili tukuze kilimo chetu kiende mbele,” Alisema.

Akimkaribisha Mkuu wa mkoa katika shamba la mmoja wa wakulima hao mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Juliet Binyura alisema kuwa watalaamu wameendelea kutoa ushauri kwa wananchi mbalimbali na hivyo kuwaomba kuendelea kufanya hivyo ili kuwasaidia wakulima kuweza kufikia kilimo chenye tija.

“Tumekuja kuangalia utaalamu aliopewa kwa wataalamu ambao ni maafisa ugani katika kata yake na wanapanda kwa kutumia kamba na wanapima vipimo vinavyokubalika naamini ya kwamba mazao atavuna vizuri,” Alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...