Ninamuagiza kila mtumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara na Taasisi zake kuhakikisha anasoma hotuba aliyotoa Mwenyekiti wa CCM taifa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, ya tarehe 12, Disemba 2019 kwenye mkutano wa Halmashauri kuu ya taifa (HKT) ya CCM uliofanyika mjini Mwanza.

Hotuba imesheheni dira, fikra na maono ambayo utekelezaji wake utaleta mageuzi makubwa ya uchumi na maendeleo ya nchi yetu na wanachi wake kufikia mwaka 2030.

Kwa muktadha huo, Wizara inafanya zoezi la kuhakikisha sera na mipango mikakati yake yote inafanyiwa mapitio ili kuongeza weledi na wigo wa Wizara kuendelea kuratibu suala zima la ujenzi wa uchumi wa kati kupitia ujenzi wa viwanda.

Tanzania ya viwanda inazidi kuonekana. Watanzania Tumemuelewa Rais wetu Magufuli, vision na political leadership yake ya kuleta mageuzi ya kiuchumi nchini. Watanzania tumeamua kutokurudi nyuma. Mashambani, viwandani, wafanyakazi, wafugaji, wavuvi, wafanyabiashara, wajasiriamali tuchape kazi. Tushike neno tutende neno ili mageuzi haya yalete heri kwenye kila kaya nchini.

By. Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara.
Dec 16, 2019

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...