NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA

KATIKA kukabiliana na wimbi la baadhi ya wenyeviti wa mitaa na vitongoji kuhusishwa na migogoro ya ardhi na rushwa  wenyeviti wapya waliochaguliwa katika uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa katika halmashauri ya Mji Kibaha, mkoani  Pwani ,wamekemewa kujihusisha na vitendo hivyo ili kurejesha imani kwa wananchi juu ya serikali yao.

Aidha wameaswa kuendelea kusimamia sheria ndogo iliyowekwa kuhusu muda wa kuruhusiwa kucheza pool na kunywa pombe kuwa ni saa kumi jioni na ambae atakiuka  sheria hiyo na mwenye baa wote wakamatwe.

Hayo aliyasema mkuu wa wilaya ya kibaha Assumpter Mshama wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa hao ambayo yameandaliwa kwa lengo la kuwajengea uwezo katika utekelazaji wa majukumu yao ikiwemo kuweka mikakati ya kupambana na migogoro ya ardhi pamoja na rushwa.

Alielezea kipindi cha nyuma wenyeviti wa mitaa walisumbua kuwa chanzo cha kuuza ardhi mara mbilimbili na wengine kusababisha migogoro ya ardhi isiyo na tija .

"Baadhi ya wenyeviti wa mitaa walichangia kuongeza changamoto ya migogoro ya ardhi,sasa msiende kuwa vinara wa kufanya waliyokuwa wakifanya wengine"

Assumpter alieleza,pia kilichowatokea wapinzani wa vyama vingine na kuacha kugombea uchaguzi wa serikali za mitaa ingekuwa vyema wakasusia na uchaguzi mkuu ujao, kuanzia kwa madiwani na wabunge ili CCM imalize kazi .

"CCM imeshajiimarisha kuanzia ngazi ya chini,ni chama gani kina mipango mizuri kama hii,yaani unakuta chama kina viongozi kuanzia kata tuu,wanakula wakubwa wanashindwa kujiimarisha kuanzia chini,na CCM tutaendelea na mwendo uleule tutashinda kwa kishindo"alifafanua Assumpter.

Nae mwenyekiti wa mtaa wa Msangani mwajuma makuka alisema wamepokea mafunzo yote waliyopewa juu ya majukumu yao na atakwenda kuyasimamia ikiwemo suala la elimu hasa kutatua changamoto za kielimu.

Wakati huo huo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mji Kibaha Jennifer Omolo alieleza lengo kubwa la kutoa mafunzo hayo ni kuweza kuwaongezea ujuzi na uwezo katika utekelezaji wa majukumu yao katika kuwasimamia wanannchi.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi ,Kibaha Mjini Maulid Bundala alisema wenyeviti wa mitaa wanawajibu wa kusimamia na kutatua changamoto za wananchi kabla ya kufika ngazi ya juu na wanapaswa kusimamia utekelezaji wa ilani ya chama hicho bila kulegalega.

Mafunzo hayo yamewashirikisha wenyeviti wa serikali za mitaa na wajumbe 438 ambapo kati yao wenyeviti ni 73  pamoja na wajumbe wake 365 kutoka katika halmashauri ya mji Kibaha na kushirikishwa viongozi mbali mbali wa serikali .
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...