Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
akizungumza na Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Regine Hess alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuona kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanywa na wataalamu kutoka JKCI, Israel na Ujerumani. Kushoto ni Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka nchini Ujerumani Felix Berger.
Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Regine Hess akizungumza
na mama wa mtoto aliyefanyiwa upasuaji mdogo wa moyo wa bila kufungua
kifua kupitia tundu dogo linalotobolewa kwenye paja wa kuziba tundu la moyo katika kambi
maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanywa na madaktari bingwa
wa Moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Israel na
Ujerumani.
Balozi
wa Ujerumani nchini Mhe. Regine Hess akizungumza na wataalamu wa afya
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Israel na Ujerumani
alipotembelea JKCI kwa
ajili ya kuona kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto wenye
matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo. Katika kambi hiyo watoto 55 walifanyiwa uchunguzi wa moyo, kati ya hao 18 walifanyiwa upasuaji mdogo wa kuziba matundu na kuzibua mishipa ya damu ya moyo iliyoziba, saba watapelekwa nchini Israel kwa ajili ya matibabu yanayohitaji utaalamu wa hali ya juu zaidi na 30 watatibiwa hapa nchini.
Daktari
bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka nchini Ujerumani Felix
Berger akimuonesha Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Regine Hess jinsi
tundu la moyo linavyozibwa kwa njia ya upasuaji mdogo wa moyo kupitia
tundu dogo linalotobolewa kwenye paja kwa kutumia mtambo wa Cathlab katika kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanywa na wataalamu kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Israel na Ujerumani.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Regine
Hess na wataalamu wa afya kutoja JKCI, Ujerumani na Israel mara baada ya balozi huyo kumaliza ziara yake ya kutembelea Taasisi hiyo ili kuona maendeleo ya kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanywa na wataalamu kutoka JKCI, Israel na Ujerumani. Katika kambi hiyo watoto 55 walifanyiwa uchunguzi wa moyo, kati ya hao 18 walifanyiwa upasuaji mdogo wa kuziba matundu na kuzibua mishipa ya damu ya moyo iliyoziba, saba watapelekwa nchini Israel kwa ajili ya matibabu yanayohitaji utaalamu wa hali ya juu zaidi na 30 watatibiwa hapa nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...