Na Yassir Simba,  Globu ya Jamii

Shirikisho la kabumbu duniani FIFA, limeipiga marufuku klabu ya Al Masry yenye maskani yake Port Said nchini Misri kutosajili katika madirisha matatu yajayo kwa kosa la kumsajili Cheick Moukoroo raia wa Ivory Coast kinyume na sheria za usajili.

Taarifa kutoka shirikisho la kandanda Misri Egyptian Football Association (EFA) limethibitisha kupokea barua hiyo ya FIFA siku ya jumanne kusema " Masry imepigwa marufuku kuingia sokoni katika  madirisha matatu yajayo kutosajili mchezaji yeye." Aidha shirikisho hilo ( FIFA) limesema kuwa klabu hiyo ya Al Masry inayo nafasi ya kukata ruhusa kuhusu adhabu hiyo.

Moukoroo mwenye umri wa miaka 28, tayari alikuwa akitumikia adhabu yake ya kutojihusisha na kandanda kwa kosa la kukatisha mkataba pasipo kuwa na makubaliano na klabu yake aliyekuwepo Al Hilal Oubeid ya  nchini Sudan katika dirisha kubwa la usajili 2017.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...