Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia utiaji saini wa mikataba ya makubaliano ya kuendesha kwa pamoja kapuni ya Twiga ya uchimbaji wa Madini kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick ambapo kwasasa kampuni mpya ya ubia ya Twiga, Serikali itakuwa na hisa ya asilimia 16 .Halfa iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Januari 24, 2020.
Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko akikidhiana mikataba na Rais wa kampuni ya Barrick Dkt. Mark Bristow iliyosainiwa mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla utiaji saini wa mikataba ya makubaliano ya kuendesha kwa pamoja kapuni ya Twiga ya uchimbaji wa Madini kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick ambapo kwasasa kampuni mpya ya ubia ya Twiga, Serikali itakuwa na hisa ya asilimia 16 Ikulu jijini Dar es Salaam. Januari 24, 2020.

Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko akiwa na Rais wa kampuni ya Barrick Dkt. Mark Bristow wakionyesha Mikataba iliyosainiwa mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla ya utiaji saini wa mikataba ya makubaliano ya kuendesha kwa pamoja kapuni ya Twiga ya uchimbaji wa Madini kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick ambapo kwasasa kampuni mpya ya ubia ya Twiga, Serikali itakuwa na hisa ya asilimia 16 Ikulu jijini Dar es Salaam. Januari 24, 2020. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mikataba ya makubaliano ya kuendesha kwa pamoja kapuni ya Twiga ya uchimbaji wa Madini kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick ambapo kwasasa kampuni mpya ya ubia ya Twiga, Serikali itakuwa na hisa ya asilimia 16 .Halfa iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Januari 24, 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mkono na Rais wa kampuni ya Barrick Dkt. Mark Bristow katika hafla ya utiaji saini wa mikataba ya makubaliano ya kuendesha kwa pamoja kapuni ya Twiga ya uchimbaji wa Madini kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick ambapo kwasasa kampuni mpya ya ubia ya Twiga, Serikali itakuwa na hisa ya asilimia 16 .Halfa iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Januari 24, 2020.
Rais wa kampuni ya Barrick Dkt. Mark Bristow akizungumza mbele ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla ya utiaji saini wa mikataba ya makubaliano ya kuendesha kwa pamoja kapuni ya Twiga ya uchimbaji wa Madini kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick ambapo kwasasa kampuni mpya ya ubia ya Twiga, Serikali itakuwa na hisa ya asilimia 16 .Halfa iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Januari 24, 2020

Wageni waalikwa wakipiga makofi mara baada yay a hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla ya utiaji saini wa mikataba ya makubaliano ya kuendesha kwa pamoja kapuni ya Twiga ya uchimbaji wa Madini kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick ambapo kwasasa kampuni mpya ya ubia ya Twiga, Serikali itakuwa na hisa ya asilimia 16 .Halfa iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Januari 24, 2020. PICHA NA IKULU


 
Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli leo Januari 24, mwaka huu wa 2020 ameshuhudia utiaji saini wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick Gold Corporation, makubaliano ambayo yameunda Kampuni ya Twiga Minerals Cooperation Limited.

Mazungumzo hayo yaliyoanza tangu mwaka 2017 hatimaye yamefika mwafaka ambapo imeundwa Kampuni ya Madini ya Twiga kwa Serikali ya Tanzania kuwa na hisa asilimia 16 na kwamba faida itakayopatikana katika kampuni hiyo, zitagawanywa asilimia 50 kwa 50 kwa manufaa ya Kampuni husika ya Twiga.

Akizungumza baada ya utiaji saini wa makubaliano hayo, Rais Magufuli amesema kuwa hiyo ni hatua kubwa kwa Watanzania baada ya mazungumzo hayo kufika mwafaka kuundwa Kampuni hiyo ya Twiga itakayokuwa na manufaa kwa Wananchi wa Tanzania katika rasilimali zao.

Rais Magufuli amesema huo ni ushindi mkubwa kwa Watanzania kutokana na hapo awali kudanganywa kuhsusu Madini hayo, "Barrick ni Kampuni kubwa duniani kufanya nao mazungumzo sio jambo dogo mwanzo Madini yalipokuwa yanachukuliwa Watanzania tuliamini ni mchanga, tunajiuliza swali kama ni mchanga kwa nini usafirishwe hadi nje ya nchi? baadae tulielewa kwamba ule haukuwa mchanga", amesema Rais Magufuli.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli ameruhusu makontena yaliyokamatwa katika Bandari ya Tanzania, amesema watafutwe Wabia yauzwe kwa faida ya Kampuni ya Twiga, Rais Magufuli amesema kama kuna mnunuzi anatakakununua Makontena hayo, ajitokeze kwa faida ya Kampuni hiyo.

Pia Rais Magufuli ameitaka Wizara ya Madini kuhakikisha inasimamia kuwapata Watanzania watakaowakilisha Taifa katika Kampuni hiyo (Twiga) wasiende kununuliwa, na kuangalia maslahi yao binafsi, badala yake waiwakilishe nchi kwa maslahi ya Taifa kwa ujumla. 

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu na Rais wa Barrick Gold, Mark Bristow amesema wamefurahi kuwepo nchini Tanzania, amesema mchakato huo haukuwa rahisi ulianza tangu 2017, ameeleza kwa sasa wamefikia mwisho na safari ya maisha bado inaendelea.

Bristow amesema Kampuni hiyo ya Twiga itawaruhusu Watanzania kuwa na maamuzi yatakayofanyika ndani ya Kampuni, amesema wanajukumu kubwa, kwa kufanya hivyo kwani sio faida yao peke yao bali faida ya wadau husuka kwa faida ya nchi husika.

Amesema Watanzania wa sasa na vizazi vijavyo wanahaki kushiriki katika taifa hili katika Migodi hiyo kwa Jamii zinazunguka kuwashirikisha zaidi katika maendeleo ya Uchumi wa Taifa.

Mikataba 9 iliyosaini mbele ya Rais kuhusu umiliki wa Hisa katika Kampuni ya Twiga mbele yako Rais Magufuli ni Mkataba wa Msingi wa Makubaliano, Mkabata wa Menejimenti na Utoaji Huduma, Mkataba wa Wanahisa wa Kampuni ya Twiga, Mkataba Wanahisa wa Kampuni ya North Mara, Mkataba wa Wanahisa wa Bulyanhulu, Mkataba wa Wanahisa wa Kampuni ya Pangea Buzwagi, Mkataba wa Maendeleo wa North Mara, Mkataba wa Maendeleo wa Bulyanhulu na Mkataba wa Maendeleo wa Pangea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...