Na Karama Kenyunko globu ya jamii.
UPANDE wa mashtaka katika kesi
ya uhujumu uchumi, inayomkabili, mwandishi wa Habari za uchunguzi Erick
Kabendera, umeieleza Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu kuwa, mchakato wa
makubaliano kati ya Kabendera na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP)
bado unaendelea.
Wakili wa Serikali Gloria Mwenda amedai hayo leo
Januari 27,2020 Mbele ya Hakimu Mkazi, Jenet Mtega wakati kesi hiyo
ilipokuja mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa.
Wakili Mwenda
amedai upelelezi bado unaendelea na mchakato wa makubaliano kwa DPP pia
unaendelea hivyo wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.
Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mtega ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 10 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.
Katika kesi hiyo, Kabendera anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji wa Sh.Mil 173.
Inadaiwa
kuwa katika kipindi hicho, Kabendera alijihusisha na mtandao wa
kihalifu kwa kutoa msaada kwa genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia
faida.
Inadaiwa kuwa katika kipindi hicho,bila ya sababu,alikwepa
kodi ya Sh 173,247,047.02 ambayo ilitakiwa ilipwe Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA).
Pia inadaiwa Kabendera alitakatisha Sh
173,247,047.02 huku akijua fedha hizo ni mazalia ya kosa la kujihusisha
na genge la uhalifu na ukwepaji kodi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...