Na Al-Hassan Muhidin,Globu ya Jamii
Mabaki ya ya miili yote tisa imepatikana katika eneo la tukio ambalo helikopta iliyokuwa imembeba gwiji wa mpira wa kikapu Kobe Brayant,mwanae Gianna na wengine saba ilianguka.
Mamlaka katika jiji la Los Angeles nchini Marekani zimesema mabaki ya mwili wa rubani pamoja na mabaki ya miili ya abiria wote nane imepatikana baada ya operesheni ya kuisaka miili hiyo kukamilika, hii ikiwa ni baada ya kuwa na Ugumu wa kuifikia eneo ambalo helikopta hiyo iliangukia kutokana na ripoti kudai kuwa chombo hicho kiliangukia eneo la ardhi lenye mteremko mrefu sana.
Hapo awali siku ya jumanne, Alex Villanueva, mmoja wa maafisa wa operesheni hiyo alisema kuwa zoezi hilo lingechukua siku kadhaa kutokana na changamoto ya eneo ambalo helikopta hio iliangukia, na leo afisa huyo amethibitisha kwamba tayari miili yote imepatikana.
Miili mitatu ilipatikana siku ya jumatatu na baada ya msako zaidi kufanyika mingine sita ikapatikana ambapo mwili wa Brayant ulitambulika kwa njia ya alama za vidole.
Wengine waliofariki katika ajali hiyo ni John Altobelli Kocha wa timu ya Baseball ya Orange Coast College, mke wake pamoja na mwanao wa kike Alyssa ambaye alikuwa akicheza timu moja ya mpira wa kikapu na mtoto wa Kobe,Gianna.
Mabaki ya ya miili yote tisa imepatikana katika eneo la tukio ambalo helikopta iliyokuwa imembeba gwiji wa mpira wa kikapu Kobe Brayant,mwanae Gianna na wengine saba ilianguka.
Mamlaka katika jiji la Los Angeles nchini Marekani zimesema mabaki ya mwili wa rubani pamoja na mabaki ya miili ya abiria wote nane imepatikana baada ya operesheni ya kuisaka miili hiyo kukamilika, hii ikiwa ni baada ya kuwa na Ugumu wa kuifikia eneo ambalo helikopta hiyo iliangukia kutokana na ripoti kudai kuwa chombo hicho kiliangukia eneo la ardhi lenye mteremko mrefu sana.
Hapo awali siku ya jumanne, Alex Villanueva, mmoja wa maafisa wa operesheni hiyo alisema kuwa zoezi hilo lingechukua siku kadhaa kutokana na changamoto ya eneo ambalo helikopta hio iliangukia, na leo afisa huyo amethibitisha kwamba tayari miili yote imepatikana.
Miili mitatu ilipatikana siku ya jumatatu na baada ya msako zaidi kufanyika mingine sita ikapatikana ambapo mwili wa Brayant ulitambulika kwa njia ya alama za vidole.
Wengine waliofariki katika ajali hiyo ni John Altobelli Kocha wa timu ya Baseball ya Orange Coast College, mke wake pamoja na mwanao wa kike Alyssa ambaye alikuwa akicheza timu moja ya mpira wa kikapu na mtoto wa Kobe,Gianna.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...