Naibu Waziri wa Nishati, Subira
Mgalu,akitia saini kwa kutumia kifaa maalum,ikiwa ni kuridhia
Makubaliano ya Sekta ya Nishati yaliyokubaliwa katika Mkutano wa Baraza
na Mawaziri wa Afrika Mashariki.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira
Mgalu (wapili kulia) akichangia mada katika Mkutano wa Baraza na
Mawaziri wa Afrika Mashariki wakati wa majadiliano ya sekta ya Nishati
kwa nchi wanachama
Naibu Waziri wa Nishati, Subira
Mgalu (wa pili kushoto) na Watendaji wakuu wa Wizara ya Nishati na
Taasisi zilizochini yake wakifuatilia Majadiliano ya Mkutano wa Baraza
la Mawaziri wa Sekta ya Nishati katika nchi za Afrika Mashariki
unaofanyika kwa njia ya mtandao,ambapo hapa nchini ulifanyika Jijini
Dodoma.
…………………………………………..
Na Zuena Msuya, Dodoma
Naibu Waziri wa Nishati, Subira
Mgalu, amesaini makubaliano ya Sekta ya Nishati ya mkutano wa Baraza na
Mawaziri wa Afrika Mashariki kwa niaba ya Waziri ya Waziri wa Nishati,
Dkt. Medard Kalemani.
Mkutano huo umefanyika Januari
14, 2019, ambapo kila nchi huufanya nchini kwake, hapa nchini mkutano
huo umefanyika jijini Dodoma kwa kushirikisha Viongozi Waandamizi wa
Wizara ya Nishati, Mashirika pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizochini ya
Wizara hiyo.
Majadiliano ya Mkutano huo
huendeshwa kwa njia ya mtandao (Video Conference) kwa kuwakutanisha
Mawaziri wa sekta husika kutoka nchi zote wanachama.
Mkutano huo hujadili taarifa
mbalimbali iliyowasilishwa kwao na Makatibu Wakuu wa Wizara husika
katika sekta hiyo zinayohusu miradi mbalimbali ya maendeleo ya Sekta ya
Nishati katika nchi wanachama.
Taarifa hiyo ya Makatibu Wakuu,
iliyowasilishwa kwa Mawaziri hayo imezungumzia masuala mbalimbali
yanayohusu Umeme, Nishati Jadidifu, Mafuta pamoja Gesi.
Baada ya majadiliano hayo,
Mawaziri wote wa Sekta ya Nishati wa nchi wanachama wa wameridhia na
kusaini makubaliano ya kisekta, kwa lengo la utekelezaji.
Mawaziri walioshiriki mkutano huo ni kutoka nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda pamoja na Burundi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...