Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, amesaini makubaliano ya Sekta ya Nishati ya mkutano wa Baraza
na Mawaziri wa Afrika Mashariki kwa niaba ya Waziri ya Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani.
Kikao hicho kinatokana taarifa ya Makatibu wakuu wa Wizara husika inayokuwa inazungumzia miradi ama uboreshaji wa sekta ya Nishati katika nchi hizo.
Taarifa hiyo, huwasilishwa katika ngazi ya Mawaziri kwa hatua zaidi, baada ya makatibu wakuu hao kuafikiana kile walichokikusudia katika nchi zao.
Baada ya majadiliano na kuafikiana na kukubaliana kile walichokikusudia kuhusiana na sekta husika, mawaziri hao huidhinisha na kutia saini tayari kwa utekelezaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...