Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara
ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Kemilembe Mutasa
akiongea wakati wa kumkaribisha Mgeni Rasmi katika Warsha ya mafunzo ya
kurejeleza gesi zilizotumika na madhara yatokanayo na matumizi ya gesi
feki kwa Wakufunzi wa Vyuo vya VETA Tanzania wanaojihusisha na
kuhudumia viyoyozi na mafriji. Warsha hiyo ilifanyika katika Chuo cha
VETA- Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana Faraja Ngerageza ambaye
ni Mgeni Rasmi katika Warsha ya mafunzo ya kurejeleza gesi zilizotumika
na madhara yatokanayo na matumizi ya gesi feki kwa Wakufunzi wa vyuo
vya VETA kutoka mikoa yote ya Tanzania akifungua warsha hiyo
iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na UNIDO.
Sehemu ya Washiriki wa Warsha ya
mafunzo ya kurejeleza gesi zilizotumika na madhara yatokanayo na
matumizi ya gesi feki kwa Wakufunzi wa vyuo vya VETA nchini
iliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha VETA – Dar es Salaam wakifuatilia
kwa makini mafunzo yaliyokua yakitolewa katika warsha hiyo.
Mgeni Rasmi katika Warsha ya
mafunzo ya kurejeleza gesi zilizotumika na madhara yatokanayo na
matumizi ya gesi feki ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mazingira
kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana Faraja Ngerageza akiwa katika
picha ya pamoja na Wajumbe waliohudhuria warsha hiyo iliyoandaliwa na
Ofisi ya Makamu wa Rais na UNIDO
……………….
Matokeo ya kuharibika kwa Tabaka
la Ozoni ni kuruhusu mionzi zaidi ya urujuani (UV-B) kufikia uso wa
ardhi hivyo kutishia afya ya viumbe hai katika ikolojia mbalimbali.
Tafiti zimethibitisha kuwa kumong’onyoka kwa tabaka la ozoni kumetokana
na kurundikana angani kwa kemikali/gesi zinazotumika kwenye mafriji,
viyoyozi na mitambo ya kupoozea joto.
Hayo yamesemwa na Kaimu
Mkurugenzi waIdara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana Faraja
Ngerageza jijini Dar es Salaama wakati akifungua warsha ya mafunzo ya
kurejeleza gesi zilizotumika na madhara yatokanayo na matumizi ya gesi
feki iliyotolewa kwa Wakufunzi wa VETA.
Alisema kuwa Serikali
imeaandaa Programu mbali mbali kwa ajili ya utekelezaji wa Itifaki ya
Montreal.
Mkakati wa kitaifa chini ya mipango ya nchi ni pamoja na:
-Kuimarisha uwezo wa Taasisi zinazohusika na utekelezaji wa Itifaki ya
Montreal, Kukusanya takwimu za uingizaji na matumizi ya kemikali
zinazoharibu tabaka la ozoni, Uhamasishaji juu ya umuhimu wa kulinda
tabaka la ozoni, Kujenga uelewa kwa Wakufunzi juu ya urejelezaji wa gesi
iliyokwisha tumika katika mafriji, viyoyozi na mitambo ya kupozea joto,
Kuhamasisha matumizi ya kemikali rafiki kwa tabaka la ozoni na Kuweka
utaratibu wa udhibiti wa uingizaji na matumizi ya kemikali zinazoharibu
tabaka la ozoni.
Ofisi
ya Makamu wa Rais imekua na utaratibu wa mara kwa mara kuandaa warsha
za mafuzo ya aina hiyo kwa Wakufunzi wa vyuo vya VETA Nchini
wanaohusika na masuala ya mafriji, viyoyozi na mitambo ya kupoozea joto.
Washiriki wa warsha hiyo wametoka katika vyuo vya VETA vifuatavyo Dar
es Salaam, Zanzibar, Kilimanjaro, Arusha, Mbeya, Mwanza, Morogoro, Pwani
na Kigoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...