Mkurugenzi wa Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadam (NIMR) Profesa  Yunus Mgaya akizungumza na waandishi wa habari na Maafisa habari wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kuhusiana na mafanikio ya Taasisi hiyo wa kipindi cha miaka minne ya uwekezaji wa serikali katika vifaa na miundombinu mbalimbali .
 Mkurugenzi wa NIMR –Muhimbilli  Profesa Sayoki Mfinanga akitoa maelezo kuhusiana na utafiti wa wanaofanya katika kituo cha Muhimbili na mafanikio yake katika utoaji wa hudumba bora kwa wananchi.
 Msanifu wa Maabara wa NIMR –Muhimbili  Said Omary akitoa maelezo ya utafifi wa kupima usugu wa vimelea ya kifua kikuu kwa dawa zinazotumika kutibu kifua hatua kwa hatua pamoja  kujua uoteshaji wa vimelea.
 Maabara yenye vifaa  vya kisasa katika upimaji wa usugu wa vimelea ya kifua kikuu kwa dawa unaofanywa kwa kuchukua sampuli katika kanda tano.
 Maabara ya sampuli NIMR-Muhimbili
Picha pamoja na watendaji wa NIMR –Muhimbili  pamoja Maafisa habari wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.


 Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) katika miaka mine ya  serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dkt.John Magufuli imeongeza tafiti kutoka 10 hadi 20 kufikia nwaka 2017.
Tafiti ambazo zimefanyika katika Taasisi hizo zimeweza  kufanya serikali kubadilisha sera ikiwamo shirika la afya Duniani (WHO)  kuunda sera ya kutumia michanganyiko ya dawa  za  kutibu ugonjwa wa mgongo unaosabishwa na fangasi .
Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na timu ya Maafisa Habari  wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Profesa Yunus Mgaya amesema kuwa NIMR-Muhimbili katika katika kutekeleza majukumu yake imefanikiwa kufanya tafiti mbalimbali kwenye magonjwa yasiyoambukiza Kifua Kikuu na vimelea vya Ukimwi na Magonjwa yasiyoambukiza.
Amesema kuwa kituo cha Muhimbili kinashirikiana na mpango wa Taifa wa  Kudhibiti Kifua Kikuu katika uboreshaji wa vipima vya maabara ya kitaifa ya kifua kikuu kwa kupima usugu wa vimelea ya kifua kikuu kwa dawa zinazotumika kutibu kifua na majibu yake yanatoka ndani siku mbili tofauti na awali majibu yalikuwa yanatoka kwa kwa miezi miwili.
Profesa Mgaya  amesema utafiti mwingine ni ule wa homa ya uti wa mgongo inayosababishwa na fangasi kwa wagonjwa wenye maambukizi ya vitusi vya ukimwi ambapo homa hiyo husababisha asilimia 25 kwa wagongwa wenye VVU.
Amesema kuwa baada ya utafiti huo kukamilika walifanya tathimini ya mkakati wa tiba wa kupunguza vifo vya wagonjwa wenye maambukizi ya fangasi na kusababisha homa ya uti wa mgongo kwa wagonjwa waliothirika na UKIMWI umepunguza vifo vya wastani wa robo tatu ya kila wagonjwa 100 wanaotibiwa /
Aidha amesema kuwa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo unasababishwa na fangasi kwa wenye VVU zamani ulikuwa unapunguza vifo kwa wastani  robo moja tu ya kila wagonjwa 100 wanaotibiwa  homa hiyo. 
Amesema utafiti wa homa ya uti wa mgongo unaosababishwa  na Fangasi kwa wagonjwa wa Ukimwi ulifanyika katika nchi za Tanzania na Zambia ulihusisha jumla ya watu wenye VVU 1999 wenye maambukizi ya fangasi kwenue damu lakini ambao maambukizi hayo hayajafikia kiwango cha kusababisha homa ya uti wa mgongo utafiti ulionyesha kupunguza vifo kwa asilimia 30 ukilinganishwa na utaratibu wa zamani kutumia tiba-kinga kwa waathirika.
Profesa  Mgaya amesema Seikali imetoa sh.800 kwa ajili ya mashine ya kutenheneza  dawa zitokanazo  na miti ambapo  tafiti zimeshafanyika na wataanza na magonjwa mawili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...