Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai
(wa pili kulia) akimvalisha na kumkabidhi joho Mhe. Pius Msekwa
alilokuwa akitumia wakati akiwa Spika wa Bunge la Nane Bungeni Jijini
Dodoma. Kulia ni Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai
(katikati waliokaa) katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Wabunge nje ya
ukumbi wa Bunge baada ya wa Sherehe fupi za kukabidhiana majoho kwa
Maspika wastaafu zilizofanyika leo Bungeni Jijini Dodoma. Kuanzia kulia
waliokaa ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Spika Mstaafu,
Mhe. Anne Makinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Kassim Majaliwa, Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa, Mbunge wa Urambo Mhe.
Margaret Sitta na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai
(katikati) katika picha ya pamoja na Maspika wastaafu ambao ni Mhe. Anne
Makinda (wa pili kushoto) na Mhe. Pius Msekwa (wa pili kulia) baada ya
Sherehe fupi za kukabidhiana majoho kwa Maspika hao zilizofanyika leo
Bungeni Jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia
Ackson na Mbunge wa Urambo, Mhe. Margaret Sitta.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai
akimkabidhi joho Mhe. Margaret Sitta kwa niaba ya mume wake aliyekuwa
Spika wa Bunge la 9 Mhe. Samuel Sitta wakati wa Sherehe fupi za
kukabidhiana majoho kwa Maspika wastaafu zilizofanyika leo Bungeni
Jijini Dodoma. Kulia ni Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai
akimpa mkono wa pongezi Spika wa Bunge la Kumi Mhe. Anne Makinda baada
ya kumkabidhi joho alilokuwa akitumia wakati akiwa Spika wa Bunge la
Kumi.PICHA NA BUNGE
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...