Mtaalamu wa utoaji wa huduma ya dharula wa Shirika la Cardiostart
International la nchini Marekani Mike Pyorala akiwafundisha baadhi ya
wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jinsi ya kutoa huduma
ya dharula kwa mtu aliyepata tatizo la ghafla la kiafya. Wataalamu wa
Shirika hilo wako JKCI kwa ajili ya kambi maalum ya upasuaji wa moyo kwa
watoto na watu wazima
Daktari bingwa wa huduma ya dharula wa Shirika la Cardiostart
International la nchini Marekani Richard Harper akiwafundisha baadhi ya
wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jinsi ya kutoa huduma
ya dharula kwa mtoto aliyepata tatizo la ghafla la kiafya. Wataalamu
wa Shirika hilo wako JKCI kwa ajili ya kambi maalum ya upasuaji wa moyo
kwa watoto na watu wazima.
Baadhi ya wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
wakimsikiliza Prof. Aubyn Marath ambaye ni daktari bingwa wa upasuaji wa
moyo (hayupo pichani) wa Shirika la Cardiostart International la nchini
Marekani wakati akiwafundisha jinsi ya kutoa huduma ya dharula kwa
mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa moyo. Wataalamu wa Shirika hilo wako
JKCI kwa ajili ya kambi maalum ya upasuaji wa moyo kwa watoto na watu
wazima.
Prof. Aubyn Marath ambaye ni daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Shirika la Cardiostart International la nchini Marekani akiwafundisha baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jinsi ya kutoa huduma ya dharula kwa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa moyo. Wataalamu wa Shirika hilo wako JKCI kwa ajili ya kambi maalum ya upasuaji wa moyo kwa watoto na watu wazima. Picha na JKCI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...