Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua
Gwaride la Heshma lililoandaliwa na Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la
Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kundi la 67/19 kabla ya kuwatunuku Kamisheni
kuwa Maofisa katika Cheo cha Luteni Usu katika hafla iliyofanyika
katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwatunuku
Kamisheni katika Cheo cha Luteni Usu Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la
Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kundi la 67/19 katika hafla iliyofanyika
katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakivalishana vyeo vipya mara baada ya kutunukiwa Kamisheni katika Cheo cha Luteni Usu na Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla
iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania (CDF) Jenerali Venance Mabeyo, Naibu Spika Tulia Ackson, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi, Viongozi mbalimbali wa Jeshi la Wananchi pamoja na Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kundi la 67/19 mara baada ya kuwatunuku Kamisheni Ikulu jijini Dar es Salaam.
iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania (CDF) Jenerali Venance Mabeyo, Naibu Spika Tulia Ackson, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi, Viongozi mbalimbali wa Jeshi la Wananchi pamoja na Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kundi la 67/19 mara baada ya kuwatunuku Kamisheni Ikulu jijini Dar es Salaam.
Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la Wananchi
wa Tanzania (JWTZ) kundi la 67/19 wakiondoka katika
viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya
kutunukiwa Kamisheni katika Cheo cha Luteni Usu na Amiri Jeshi
Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Magufuli.
Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la Wananchi wa
Tanzania (JWTZ) wakila Kiapo cha Utii kwa Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kuwatunuku Kamisheni Ikulu jijini Dar es Salaam.
PICHA NA IKULU
Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli katika Hafla ya kutunuku kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi 128 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) iliyofanyika Ikulu Jijini
Dar es Salaam leo Februari 8, 2020, ambapo kati ya hao 108 ni Wanaume na 20 ni wanawake.
Kikundi cha Ngoma kutoka Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa Makutupola Jijini Dodoma, kikitoa burudani katika hafla ya kutunuku kamisheni ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam leo Februari 8, 2020.
Picha na Idara ya Habari-MAELEZO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...