Katika ajali hiyo dereva wa gari ndogo T.536 DDM Toyota Carina amejeruhi na anaendelea na matibabu. Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa magari yote mawili katika eneo la makazi ya watu.
Aidha katika ajali hiyo magari yote mawili yameharibika na Tanker la Mafuta liliacha njia na kwenda kugonga maduka ya bidhaa mbalimbali yaliyopo kando kando ya barabara.
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama lipo eneo la tukio kuhakikisha mafuta yaliyopo katika gari lililopata ajali yanahamishiwa kwenye gari lingine bila kusababisha madhara yoyote ikiwa ni pamoja na jitihada za kuliinua tanker la mafuta lililoacha njia na kupinduka.
Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...