Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akihakiki taarifa zake za mpiga kura kwenye Daftari la Wapiga
kura katika Kituo cha Shule ya Sekondari SOS Wilaya ya Magharibi (B)
Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo Febuari 27,2020. katikati ni
Mkurugenzi wa tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC Thabit Idarous Faina.
Afisa wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Jamii Zanzibar Khatib Said
Bakari akimkabidhi Kitambulisho cha Mzanzibari Mkazi Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Febuari
27,2020 Tunguu Zanzibar Baada ya kuhakikiwa upya kwa Vitambulisho
hivyo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akionesha Kitambulisho Kipya cha Mzanzibari Mkaazi baada kukabidhiwa kitambulisho hicho na Afisa wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Jamii Zanzibar Khatib Said Bakari leo Febuari 27,2020 Tunguu Zanzibar. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...