NA MWAMVUA MWINYI,BAGAMOYO
WAKAZI
wa Vijiji na Vitongoji ,vinavyounda kata Jimbo la Bagamoyo Mkoani
Pwani, watanufaika na usambazaji wa maji kutoka kwenye vyanzo vilivyopo
kweye maeneo yao,kupitia mradi wa maji Chombe Juu.
Hayo
yalibainishwa na Mbunge wa Jimbo hilo Dkt. Shukuru Kawambwa,
akizungumza na wakazi wa Kitongoji cha Chombe Juu Kata ya Yombo,
aliposhuhudia matofari na mabomba yatayojenga kituo cha kuchotea maji na
mabomba ya kusambazia kwenye vituo vitatu.
Alisema
, serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli, imedhamira
kuwakomboa wananchi kwa kuwaondolea kero ya ukosefu wa maji safi na
salama.
"Hapa
nilileta wadau kuchimba visima viwili kwa thamani ya zaidi ya
sh.milioni 9, lakini kwa bahati mbaya maeneo hayo moja halikuwa na maji "
alisema Dkt. Kawambwa.
Mhandisi
wa maji (RUWASA)James Kionaumela aliishukuru serikali kwa kuanzisha
chombo kinachoitwa RUWASA, kinacholenga kushughulikia usambazaji wa maji
kutoka kwenye vyanzo na kuwasambazia wananchi.
Alielez,
wamepewa jukumu la kuwasambazia maji wananchi, kutoka katika visima na
kutandaza mabomba ili maji hayo yawafikie wananchi, na Chombe Juu
wanapeleka matofali na mabomba kwa ajili ya kazi hiyo.
Makamu
Mwenyekiti wa halmashauri ya Bagamoyo, Mohammed Usinga alisema kuwa
juhudi hizo zinalenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji.
"Tulikuja
kutoka ahadi ya maji katika eneo hili, leo tumefika hapa chini ya Mkuu
wetu wa msafara Dkt. Shukuru Kawambwa anayefanyakazi kubwa ya kuwatafuta
marafiki kwa ajili ya kiiendeleza mradi wa maji uliopo kwnye eneo
hill," alisema Usinga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...