Serikali ya Awamu ya Tano imepongezwa kwa kuwezesha wananchi kufikiwa na huduma ya majisafi na salama baada ya miaka zaidi ya hamsini bila kuwepo kwa huduma hiyo katika eneo lao.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso mwishoni mwa wiki wakati akizindua mradi wa maji katika jijiji cha Makang’a, jimbo la Mtera mkoani Dodoma utakaonufaisha wananchi zaidi ya elfu saba na mia tano.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso mwishoni mwa wiki wakati akizindua mradi wa maji katika jijiji cha Makang’a, jimbo la Mtera mkoani Dodoma utakaonufaisha wananchi zaidi ya elfu saba na mia tano.
“Mradi huu umetumia milioni 350 tu wakati tungetumia mkandarasi ingetumia zaidi milioni 600 na utaleta mageuzi makubwa ya kiuchumi katika eneo lenu na hii ndiyo dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano kuhakikisha kuwa wananchi wote mnapata maji safi na salama,” alisisistza Aweso.
Akifafanua, Naibu Waziri Aweso amesema kuwa mradi huo umetekelezwa na wataalamu wa ndani kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (DUWASA) ikiwa ndio dhamira ya Serikali kupitia Wizara ya maji kutekeleza miradi ya maji hasa vijijini kwa kutumia wataalamu wa ndani.
“Serikali ya Awamu ya Tano inawajali wananchi wake hivyo pamoja na kukamilika kwa mradi huu tumeshatoa fedha nyingine kiasi cha shilingi milioni miamoja ziko kwenye akaunti tayari kwa ajili ya kuchimba visima viwili, hivyo wataalamu wetu watakuja hapa jumatatu tarehe 11 kufanya utafiti wa maeneo vitakapochimbwa visima hivyo”, alisisitiza Aweso.
Wananchi wote hakikisheni mnautunza mradi huu ili unufaishe hata vizazi vijavyo kwa kuwa fedha nyingi zimetumika katika kuutekeleza.
Naye, Mkurugenzi wa DUWASA Mhandisi David Palangyo amesema kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa tarehe 19 Septemba2019 na umehusisha ujenzi wa vituo kumi na tatu (13) vya kuchotea maji kwenye maeneo mbalimbali katika Kijiji hicho, kununua na kufunga pampu zenye uwezo wa kuzalisha lita laki tatu na thelathini na sita kwa siku, mfumo wa nguvu za jua kwa ajili ya kuendesha pampu hizo, ununuzi na ulazaji wa mabomba ya plastiki na viungio vyake.
Kazi nyingine ni uchimbaji na ufukiaji wa mabomba ya plastiki ya class C na viungio vyake na kulaza mabomba yenye vipenyo vya ichi 1.5 hadi inchi 6 kwa jumla ya urefu wa meta zaidi ya elfu kumi na tatu.
Akizungumzia mafaniko ya mradi huo, Mhandisi Palangyo amesema kuwa wananchi wote wa Kijii cha Makangw’a sasa wanapata maji ya bomba na pia wananchi walishirikishwa katika mradi huo kuanzia kuchagua maeneo ya kujenga vituo vya kuchotea maji na hata utekelezaji wa mradi huo.
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo hilo Livingstone Lusinde amesema kuwa wananchi wanaonufaika na mradi huo wanaowajibu wa kutunza mradi huo ili usihujumiwe.
Kwa upande wa viongozi watakaosimamia mradi huo wametakiwa kuhakikisha
wanasoma mapato na matumizi ya mradi huo na kutunza fedha zitakazotokana
na mradi huo benki ili uwe endelevu.
Kabla ya kutekelezwa kwa mradi huo hali ya upatikanaji wa maji katika Kijiji cha Makangw’a ilikuwa siyo wa kuridhisha, maji ya bomba yalikuwa yanapatikana katika kitongoji kimoja tu kati ya 11 na yaliwekwa na mwekezaji binafsi mwaka 2016.
Kabla ya kutekelezwa kwa mradi huo hali ya upatikanaji wa maji katika Kijiji cha Makangw’a ilikuwa siyo wa kuridhisha, maji ya bomba yalikuwa yanapatikana katika kitongoji kimoja tu kati ya 11 na yaliwekwa na mwekezaji binafsi mwaka 2016.
Naibu Waziri wa Maji, mhe. Jumaa Aweso akizungumza kwa furaha wakati
akizindua mradi wa maji utakaonufaisha wakazi zaidi ya elfu saba na
miatano katika kijiji cha Makang’wa jimbo la Mtera mkoani Dodoma
Februari 8, 2020.
Naibu Waziri wa Maji, mhe. Jumaa Aweso akizindua mradi wa maji
utakaonufaisha wakazi zaidi ya 7500 katika kijiji cha Makang’wa jimbo la
Mtera mkoani Dodoma Februari 8, 2020.
Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira
Dodoma (DUWASA) Mhandisi David Pallangyo akitoa maelezo kuhusu
utekelezaji wa mradi wa maji utakaonufaisha wakazi zaidi ya elfu saba
na miatano katika kijiji cha Makang’wa katika jimbo la Mtera mkoani
Dodoma Februari 8, 2020.
Mbunge wa jimbo la Mtera mkoani Dodoma, Mhe. Livingstone Lusinde
akishukuru Serikali na Mamalaka ya Maji na Usafi wa mazingira Dodoma
(DUWASA) kwa kuendelea kutatua changamaoto ya upatikanaji wa maji katika
jimbo hilo wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji utakaonufaisha wakazi
zaidi ya 7500 katika kijiji cha Makang’wa jimboni humo Februari 8,
2020.
Kwaya ya Kijiji cha Makang’wa katika jimbo la Mtera ikitumbuiza wakati
wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa maji utakaonufaisha wakazi zaidi ya
Elfu saba na miatano katika kijiji cha Makang’wa katika jimbo hilo
Februari 8, 2020.
Naibu Waziri wa Maji, mhe. Jumaa Aweso akiwa amebeba ndoo ya maji
baada ya kuzindua mradi wa maji utakaonufaisha wakazi zaidi ya 7500
katika kijiji cha Makang’wa jimbo la Mtera mkoani Dodoma Februari 8,
2020.Fedha za utekelezaji wa mradi huo zimetolewa na Serikali kuptia
Wizara ya maji na mradi kutekelezwa na DUWASA.
Wananchi wa kijiji cha Makang’wa jimbo la Mtera mkoani Dodoma
wakifuatilia hotuba ya uzinduzi wa mradi wa maji katika Kijiji chao
Februari 8, 2020, Mradi huo utanufaisha wakazi zaidi ya 7500 wa kijiji
hicho.
Naibu Waziri wa Maji mhe. Jumaa Aweso akisisitiza jambo kwa. Mbunge
wa jimbo la Mtera mkoani Dodoma Mhe. Livingstone Lusinde baada ya
kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Makang’wa jimboni humo.
Meneja ufundi kutoka DUWASA mhandisi Mayunga Kashilimu akitoa maelezo
kwa Naibu Waziri wa Maji mhe. Jumaa Aweso kuhusu utekelezaji wa mradi
wa maji katika kijiji cha Makang’wa jimbo la Mtera mkoani Dodoma
Februari 8, 2020 wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi huo.Fedha za
utekelezaji wa mradi huo zimetolewa na Serikali kuptia Wizara ya maji na
mradi kutekelezwa na DUWASA.
Mbunge wa jimbo la Mtera mkoani Dodoma, Mhe. Livingstone Lusinde (kulia)
akisisitiza jambo kwa Naibu Waziri wa Maji mhe. Jumaa Aweso wakati
wa uzinduzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Makang’wa jimboni humo.
Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira
Dodoma (DUWASA) Mhandisi David Pallangyo (kushoto) akisisitiza jambo
kwa Naibu Waziri wa Maji mhe. Jumaa Aweso wakati wa uzinduzi wa
mradi wa maji katika kijiji cha Makang’wa jimbo la Mtera, Mradi huo
unanufaisha wananchi zaidi ya elfu saba na miatano.
Naibu Waziri wa Maji mhe. Jumaa Aweso akimtwisha ndoo ya maji mmoja
wa wakazi wa kijiji cha Makangw’a katika jimbo la Mtera mkoani Dodoma
baada ya kuzindua mradi huo Februari 8, 2020.
Naibu Waziri wa Maji mhe. Jumaa Aweso akiwa amebeba ndoo ya maji katika kijiji cha Makang’wa jimbo la Mtera,baada ya kuzindua Mradi huo unaonufaisha wananchi zaidi ya elfu saba na miatano.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...