Katibu Mkuu Dkt.Zainab Chaula wakikabidhiana ripoti ya hospitali ya rufaa ya mkoa maweni na Katibu Tawala wa mkoa wa kigoma Rashid Machatta.
Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula akimkabidhia Mhasibu Mkuu wa Wizara ya afya Hellen Mwakipunda ripoti hiyo.
Katibu Mkuu wizara ya afya Dkt. Zainab Chaula akisaini ripoti ya taarifa ya hospitali ya rufaa ya mkoa ya maweni,makabidhiano hayo yalifanyika kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa wa kagera
Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Rashid Mchatta akisaini ripoti ya makabidhiano ya hospitali ya rufaa ya mkoa maweni, kushoto akishuhudiwa na Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula


…………………………………………………………

Na. Catherine Sungura– Kigoma

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imekabidhiwa rasmi hospitali ya rufaa ya mkoa maweni iliyopo mkoani hapa.

Akikabidhiwa hospitali hiyo Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa anashukuru sekretarieti ya mkoa kwa kuisimamia hospitali hiyo pamoja na watumishi katika kipindi hicho na hivyo kuwezesha wananchi kupata huduma zinazostahili.

“Pamoja na makadhibiano tutaendelea kushirikiana kwa ukaribu na ofisi yako RAS na bado utaendelea kuwasimamia watumishi hawa kwani wapo mkoani kwako”.

Aidha, Dkt. Chaula amesema wizara yake wametengeneza mkataba kati ya Wizara na RAS katika eneo la usimamizi hasa ya majengo ili yaweze kubaki kwenye uimara unaohitajika.

“Tunawashukuru watendaji wa ofisi ya katibu tawala kwa kazi nzuri waliyoifanya ya usimamizi wa hospitali hiyo hadi sasa tunakabidhiana, tutakwenda kuzisoma nyaraka hizi moja baada ya nyingine, maana ni mali za Serikali, mmetueleza kuna madeni tutayapitia na kuyafanyia kazi,” alisema.

Naye Katibu Tawala wa mkoa wa kigoma Rashid Machatta alisema kwamba bado ataendelea kushirikiana kwa ukaribu na watumishi wa hospitali hiyo katika utekelezaji wa majukumu yao ili wananchi waweze kupata huduma bora

“ Watumishi sisi bado ni wamoja, tutashirikiana bega kwa bega ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata huduma zilizo bora”.Alisema Rashid Machatta.

Wakati huo huo Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Osmond Dyegula alisema hospitali hiyo ina jumla ya watumishi 233, kwa wastani wanaona wagonjwa kati ya 300 hadi 330 kwa siku kutokana na takwimu za mtuha za mwaka 2018/19.

Wizara ya afya imekabidhiwa hospitali hiyo ikiwa ni agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kuhamishia usimamizi huo wizara ya afya mwaka 2017 kutoka chini ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...