Afrika Kusini imekuwa nchi ya hivi punde ya chini ya jangwa la Sahara barani Afrika kuthibitisha kuwa na mtu anayeugua homa inayosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19).

Akizungumza masaa machache baada ya kuthibitishwa kesi hiyo ya kwanza ya Corona nchini Afrika Kusini, Rais Cyril Ramaphosa wa nchi hiyo amesema kuingia kwa ugonjwa huo hatari kutakuwa na taathira hasi kwa sekta ya utalii na uchumi wa nchi hiyo ambao tayari unayumba.

Ameongeza kuwa, "tutazidi kuwataarifu Waafrika Kusini kwa uwazi kuhusu hatua tulizochukua, kwa kuwa kesi hii huenda ikageuka na kuwa mgogoro wa kitaifa."

Awali, Waziri wa Afya wa nchi hiyo, Zweli Mkhize aliliambia Bunge kuwa, aliyekumbwa na Corona ni mwaume wa miaka 38, aliyekuwa amesafiri kwenda Italia pamoja na mkewe na kisha kurejea nchini humo wakiwa pamoja na watu wengine 10 mnamo Machi Mosi. Waziri huyo ameongeza kuwa, tayari watu hao wamewekwa katika karantini ili kuzuia maambukizi zaidi.

Kabla ya Afrika Kusini, nchi nyingine za Afrika ambazo zimethibitisha kuwa na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona ni Algeria, Misri, Morocco, Nigeria, Senegal na Tunisia.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...