Na
Amiri kilagalila,Njombe
Mzee
Arusha Nziku (75) mkazi wa wilaya ya Wanging’ombe mkaoni Njombe,amekutwa
amefariki nyumbani kwake huku akiwa amefungwa kamba ndani ya nyumba yake
kuonyesha emejinyonga.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Njombe Hamisi Issa amesema waliotekeleza mauaji hayo walitumia
kamba kumfunga na kuonyesha kama amejinyonga.
“Ni
mzee ambaye amekufa akiwa nyumbani kwake na hawa wauaji walichokifanya ni
kwamba baada ya kumuua wakamfanya kama amejinyonga,ile kamba wameifunga lakini
kwa ufupi wa lile jingo na urefu wa ile kamba inaonyesha kifo ni cha mashaka”alisema
Hamis Issa
Aidha
amesema mpaka sasa jeshi la polisi limeingia kazini kuhakikisha ni kitu gani
kilicho sababisha kifo cha mzee huyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...