MKUTANO wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya
Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umefanyika leo jijini Dar es Salaam kwa njia ya Mtandao (Video Conferencing) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC)  Mkutano huo umefunguliwa na

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Maafisa Waandamizi/ Makatibu Wakuu, Balozi Kanali Wilbert Ibuge Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Wajumbe wengine ni waliohudhuria ni Katibu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Prof. Abel Makubi, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utaii Dkt. Aloyce Nzuki pamoja
na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipago, Bi Amina K. Shaaban.
Mkutano wa Baraza la Mawaziri utafanyika Mei 29, 2020 baada ya kukamilika kwa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Maafisa Waandamizi/Makatibu Wakuu ambapo pamoja na mambo menine, Kikao cha Maafisa waandamizi kimejadili masuala mbalimbali ndani ya Jumuiya ikiwemo Mlipuko wa Virusi vya Corona ndani ya SADC.
Mkutano huo utaangalia utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri kilichofanyika mwezi Aprili 2020 kuhusu COVID 19 na athari zake katika utekelezaji wa programu za SADC, athari za kijamii na kiuchumi za COVID -19 na madhara yake ndani ya Jumuiya.
Aidha, Mkutano huu pia umejadili Hali ya kifedha ndani ya Jumuiya, Utekelezaji wa Maazimio yaliyotokana na kikao cha Baraza la Mawaziri wa SADC ambayo ni Menejimenti ya Maafa, utekelezaji wa kaulimbiu ya Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC isemayo "Mazingira Wezeshi kwa ajili ya Maendeleo Endelevu na Jumuishi ya Viwanda, Kukuza Biashara na Ajira ndani ya SADC" na mapitio ya hali halisi ya biashara baina ya nchi, maendeleo ya viwanda ndani ya Jumuiya na taarifa ya utekelezaji wa Mkakati wa Maendeleo ya Viwanda wa Jumuiya na Mpango kazi wake.
Mkutano huo umehusisha wataalamu kutoka nchi
wanachama 12 wa SADC kutoka sekta za
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Fedha na Mipango, Uchukuzi na Mawasiliano, Viwanda na Biashara, Maliasili na Utalii pamoja na Afya.
Nchi zilizoshiriki Mkutano huo ni Angola, Afrika Kusini, Comoro, Eswatini, Mauritius, Msumbiji, Madagascar, Namibia, Visiwa vya Shelisheli, Zambia, Zimbabwe na Mwenyekiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge (kushoto) akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Agnes Kayola wakati akifungua mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC kwa ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika kwa njia ya (Video Conference) leo Jijini Dar es Salaam  
 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge (aliyevaa koti jeusi) akiongea na wajumbe wa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC kwa ngazi ya Makatibu Wakuu kwa njia ya (Video Conference) leo Jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Makatibu Wakuu wakifuatilia mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC uliofanyika kwa njia ya (Video Conference) leo Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge (wa kwanza meza kuu kushoto) akiongea na wajumbe wa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC kwa njia ya (Video Conference) leo Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...