Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe (wa pili kushoto) akikabidhi msaada wa kompyuta tano na printa moja zenye thamani ya Sh.milioni 9.7 katika Shule ya Sekondari ya Ilongero iliyopo Wilaya ya Singida  mkoani Singida. Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida,  Eliya Digha, Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Mulagiri,  Diwani wa Kata ya Ilongero,  Issa Mwiru na Mkuu wa shule hiyo, Ramadhan James.
 Vifaa hivyo vikikabidhiwa. Wengine ni viongozi mbalimbali wa wilaya hiyo.
Hapa wakionesha ishara ya mshikamano.




Na Dotto Mwaibale, Singida

MBUNGE wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe ametoa msaada wa kompyuta tano na printa moja zenye thamani ya Sh.milioni 9.7 katika Shule ya Sekondari ya Ilongero iliyopo Wilaya ya Singida  mkoani Singida.

Mattembe akizungumza juzi wakati akitoa msaada huo alisema umelenga kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. John Magufuli za kuhakikisha mpango wa utoaji elimu bure kwa kila mtoto hapa nchini unaendelea kufanikiwa.

" Niliona ni muunge mkono Rais wetu kwa kutoa msaada huu kwa wanafunzi wetu hawa wa Sekondari ya Ilongero kusoma masomo ya ICT  kwa njia ya vitendo ili waendane sanjari na ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia." alisema Mattembe.

Mattembe alisema dunia hivi sasa imepiga hatua kubwa ya maendeleo hasa katika matumizi ya teknolojia hivyo wanafunzi wetu wasipojifunza masomo ya ICT watachelewa kuyafikia mafanikio.

" Hivi sasa kila jambo linalofanyika linafanyika kwa njia ya mtandao ambapo ni lazima muhusika ajue kutumia kompyuta au simu sasa tukiacha kuwekeza katika masomo hayo itakuwa changamoto kubwa kwa watoto wetu." alisema Mattembe.

Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Mulagiri ambaye alikuwa mgeni rasmi katika makabidhiano hayo akizungumza wakati akimkabidhi msaada huo mkuu wa shule hiyo,  Ramadhan James, alisema msaada huo umekuja wakati muafaka ambao utawasaidia wanafunzi kujifunza masomo kwa ufasaha hasa kipindi hiki ambacho dunia inaunganishwa na mitandao.

"Pamoja na yote katika kipindi hiki cha ugonjwa wa Corona kompyuta hizi zitasaidia wanafunzi wetu kujifunza kwa njia ya mtandao bila ya kuwa darasani hivyo napenda kumshukuru Mhe.Mattembe kwa kuona mbali na kutoa msaada huu ambao umefika kwa wakati muafaka"  alisema Mulagiri.

Wageni waalikwa wengine katika  makabidhiano ya kompyuta hizo walikuwa ni  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida,  Eliya Digha, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi  (CCM) Wilaya ya Singida,  William Nyalandu,  Diwani wa Kata ya Ilongero,  Issa Mwiru,  Diwani Viti Maalumu wa kata hiyo, Mwanamosha Bakari, Diwani Viti Maalumu, Salma Kundya na Katibu Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Singida, Naomi David.

Wengine walioshuhudia makabidhiano hayo ni walimu wa shule hiyo,wenyeviti wa Serikali za mitaa wa Ilongero  na baadhi ya wazazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...