Mkurugenzi wa kampuni ya Ador Tanzania Ltd, Habibu Mchange akizungumza na Waandishi wa Habari Mara baada ya kuchukua na kurejesha fomu Leo. Mkurugenzi wa kampuni ya Ador Tanzania Ltd, Habibu Mchange akikabidhiwa fomu na Katibu wa CCM Wilaya ya Kibaha.Mkurugenzi wa kampuni ya Ador Tanzania Ltd, Habibu Mchange akirejesha fomu ya kuwania Ubunge jumbo la Kibaha Mjini.

***************************************
Na Mwandishi Wetu,Kibaha .

Mkurugenzi wa Kampuni ya Ador Tanzania Limited inayochapisha magazeti ya Jamvi la Habari na Times Observer, Habibu Mchange Leo amechukua na kurudisha fomu ya kugombea ubunge katika jimbo la Kibaha Mjini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi(CCM). 

Mchange amechukua na kurudisha fomu hiyo majira ya saa tisa mchana akiwa ameongozana na mkewe Zaria Abdalah Mchange . 

Akizungumza Mara baada ya kurejesha fomu hiyo mchange amesema kuwa amechukua fomu hiyo kutimiza haki yake ya kikatiba Kama Mwanachama wa CCM. 

“Nimechukua fomu Leo Kama haki yangu ya Kikatiba inavyonitaka hivyo mengine mengine yote tuwaachie vikao wao ndio watahamua” anasema Mchange.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...