Mdhibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Bw. Charles Kichere, akioneshwa
kitabu cha bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 toleo la
wananchi, na Afisa wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Juma Mfaume wakati
alipotembelea banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya
Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam ambapo Wizara ya Fedha na
Mipango na Taasisi zake inashiriki katika maonesho hayo kwa lengo la
kuwafikia wananchi na kutoa elimu na huduma mbalimbali.
Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Msafiri Mbibo akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa
wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Juma Mfaume, alipokuwa akitoa elimu
kuhusu bajeti ya Serikali na namna Serikali inavyosimamia mchakato wa
uandaaji na utekelezaji wa bajeti. Katikati ni Mkurugenzi wa Elimu kwa
Mlipakodi wa Mamlaka hiyo Bw. Richard Kayombo.
Katibu wa Bunge
Bw. Stephen Kagaigai, akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa wa Wizara ya
Fedha na Mipango Bw. Joseph Msumule alipokuwa akieleza Sera, Sheria na
kanuni za huduma ndogo za fedha zenye lengo la kuweka mazingira wezeshi
ili kurahisisha usimamizi wa huduma ndogo za fedha katika sekta ya
fedha, kutoa elimu kuhimiza watoa huduma ndogo za fedha waweze
kujisajili na kupata leseni, katika Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya
Biashara yanayoendelea katika uwanja wa maonesho wa Mwalimu Nyerere
jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Bunge
Bw. Stephen Kagaigai, akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa wa Wizara ya
Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Maendaenda, alipokuwa akitoa maelezo
kuhusu Mfumo wa Malipo ya Serikali kwa njia ya Kielektroniki (GePG)
wenye lengo la kuongeza uwazi na udhibiti wa fedha za umma, kuboresha na
kurahisisha namna ya kulipia huduma za umma, katika Maonesho ya 44 ya
Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika uwanja wa maonesho wa Mwalimu
Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Bunge
Bw. Stephen Kagaigai, akisaini daftari la wageni alipotembelea banda
la maonesho la Wizara ya Fedha na Mipango katika Maonesho ya 44 ya
Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika uwanja wa maonesho wa Mwalimu
Nyerere jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa wa Wizara hiyo Bi.
Josephine Majura.
Naibu Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Msafiri Mbibo akimsikiliza
Afisa Mwandamizi Masoko na Uhusiano kwa Umma wa Bodi ya Wataalamu wa
Ununuzi na Ugavi (PSPTB) Bi. Shamim Mdee, alipokuwa akitoa maelezo ya
huduma zinazotolewa na Bodi hiyo, wakati alipotembelea banda la Wizara
ya Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zake katika Maonesho ya 44 ya
Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Bw. Charles Kichere, akimsikiliza
Mchambuzi wa Mifumo wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bi
Siganike Baruti, alipokuwa akitoa elimu kwa umma wakati wa Maonesho ya
44 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha na Mipango)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...