Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC),
Geoffrey Mwambe amesema kuwa Miundombinu iliyojengwa na Serikali imewezesha
kituo hicho kupiga hatua kubwa na kulete wawekezaji wengi katika Sekta ya
uwekezaji hasa kwenye sekta ya Viwanda.
Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari
Jijini Dar es Salaam, Mwambe amesema miundombinu iliyojengwa na Serikali ya
Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa kipindi hiki cha miaka
mitano imekuwa ni mishipa ya kituo hicho kufanikisha sekta hiyo muhimu nchini.
“Miundombinu iliyojengwa na Serikali kwenye hii miaka
mitano sisi kwetu kama kituo cha uwekezaji inatumika kama mishipa ya damu,
kwani inapunguza gharama ya usafirishaji, kwa hiyo imetusaidia ndani ya miaka hii mitano ya Rais Magufuli
tokea Juni 2016 hadi Juni 2020 tumeweza kusajili miradi 1, 312 yenye thamani ya
dola za Kimarekani Bilioni 20”, Alisema Mwambe.
Alibainisha kuwa asilimia 54 ya miradi hiyo ipo sekta
ya viwanda ambayo imeisaidia Tanzania kuingia uchumi wa kati na katika
uwekezaji wa miradi yote asilimia 28 ni uwekezaji wa wazawa, asilimia 43 wageni
na asilimia 29 ni uwekezaji wa mashirikiano
kati ya wazawa na wageni.
Mwambe alisema kuwa katika utekelezaji wa kuimarisha
uwekezaji TIC wameanzisha ofisi zingine kikanda kusogeza huduma kwa wawekezaji
kwenye maeneo mbalimbali ya uwekezaji ikiwemo kanda ya Magharibi ikijumulisha
mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora.
Aliongeza kuwa kanda zingine ni zile za Pwani kwa
Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, lakini pia kanda ya kati yenye mikoa ya
Morogoro, Singida na Dodoma na kanda ya ziwa yenye mikoa ya Mwanza, Shinyanga,
Mara na Kagera na kanda zingine ambako kila huduma kwa
wawekezaji zinapatikana kwa urahisi.
Aidha, Mwambe alieleza mageuzi makubwa ambayo TIC wamefanya
kwa miaka mitano ya Serikali ya Awamu ya Tano Ikiwemo kuimarisha mifumo ya
huduma kwa wawekezaji kama vile Mfumo wa utoaji wa cheti cha uwekezaji kwa njia
ya kieletroniki, Mfumo wa Usajili wa makampuni na Mfumo wa Ulipaji Serikalini
(MUSE).
Mwambe alisema kuwa sekta ya uwekezaji katika viwanda
ni kubwa kuliko sekta yeyote ile kwa hiyo Serikali ya Awamu ya Tano chini ya
uongozi wa Rais Dkt.John Pombe Magufuli inatekeleza kwa vitendo Sera ya Uchumi
wa kati wenye Viwanda ambapo Julai 1, 2020 Tanzania ilitangazwa rasmi kuwa moja
ya nchi yenye uchumi wa kati duniani.
“Tumefanikisha
kwa kiasi kikubwa sana kwenye uwekezaji wa viwanda, na hii inatupa faraja sana
kuwa Serikali inatekeleza na kusimamia Sera yake ya uchumi wa Viwanda, lakini
pia tafsiri ya viwanda imeweza kuendana na uchakataji wa mazao yetu kwenye
maeneo mbalimbali nchini”, Alisema Mwambe.
Mkurugenzi
wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC),
Geoffrey Mwambe akionesha moja ya jarida linalochapishwa na kituo hicho,likieleza taarifa mbalimbali kuhusu mambo ya uwekezaji,mbele ya Waandishi wa Habari leo jijini Dar.Picha zote na Michuzi JR-MICHUZI MEDIA.
Mkurugenzi
wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC),
Geoffrey Mwambe akizungumza mbele ya Waandishi habari leo jijini
Dar,alipokuwa akitoa taarifa ya mafanikio ya kituo hicho cha TIC katika
kipindi cha miaka mitano ya Serikali ya awamu ya Tano
Baadhi ya Waandishi wa Habari na Viongozi waandamizi wa Kituo hicho wakimsikiliza Mkurugenzi
wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),
Geoffrey Mwambe alipokuwa akifafanua mambo mbalimbali ikiwemo mafaniko
ya kituo hicho kwa miaka mitano ya Rais Dkt John Pombe Magufuli.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...