Bi. Margaret Karume mwenye uzoefu wa miaka 27 kwenye sekta ya benki



 NIC Bank Tanzania Ltd na CBA Bank Tanzania Ltd wapo mbioni kumalizia uunganaji wa taasisi zao na kuanza kutoa huduma zao kama NCBA Bank Tanzania Ltd. Wajumbe wa bodi teule wamemteua Bi. Margaret Karume atakaekua Mkurugenzi na Afisa Mkuu Mtendaji wa NCBA Bank (T) kuanzia tarehe 8 Julai benki itakapoanza kutoa huduma zake rasmi.



Kwa sasa Bi. Karume ni Mkurugenzi Mkuu wa NIC Bank Tanzania mwenye uzoefu wa miaka 27 katika sekta ya benki.



‘Huu ni ukurasa mpya kwa benki hizi mbili. Natazamia kufanya kazi na timu ya watu wenye nia moja ili kuimarisha taasisi yetu ya fedha nchini Tanzania. Taasisi hii mpya itaakisi dhamira na maadili kutoka benki zote mbili, baada ya kujifunza ubora wa pande zote na kujenga taasisi kubwa na bora ya kuwahudumia wateja na wadau wetu,’’ alinukuliwa Bi. Karume.



Katika vipindi tofauti, Bi. Karume amewahi kushikilia nyazfa mbalimbali katika sekta ya benki na kuwa kiongozi wa kuigwa katika ngazi zote za chini hadi juu za benki. Alipokuwa NIC Bank Group nchini Kenya amefanya kazi kama Mkurugenzi Mtendaji wa Mikopo Hatarishi. Bi. Karume ana uzoefu imara na taaluma kwenye maendeleo ya fedha na biashara. Vilevile, ana utajiri na uzoefu katika kuhudumia wateja wakubwa wa kibenki uzoefu alioupata alipokuwa NIC Group plc na Barclays Bank Kenya (kwa sasa ABSA Bank).



Anashikilia shahada ya uzamili katika uratibu duniani (MBA ya Global Executive) na Shahada ya Sayansi (BSc). Alihitimu elimu ya utawala wa ngazi ya kibiashara kimataifa kutoka United States International University (USIU) – Africa na stashahada ya usimamizi wa mahusiano ya wateja kutoka Taasisi ya Kifedha (Uingereza). Vilevile, yeye ni mwanachama wa Taasisi ya Masuala ya Kifedha, Kenya.



Akithibitisha uteuzi wake, mwenyekiti mteule wa bodi ya NCBA Bw. Sharmapal Aggarwal alimpongeza Bi. Karume kwa kuteuliwa kwake.



‘Tunatambua uzoefu wake mkubwa kwenye sekta ya benki na tunasifu kwa kujitoa kwake upya kwenye benki. Tunaamini kuwa yeye ni mtu sahihi kuiongoza Benki ya NCBA kwenye zama mpya ya maendeleo endelevu na kuleta mafanikio kwa wadau wote Tanzania na bara la Afrika kwa ujumla,’’ alinukuliwa. Vilevile alibainisha kuwa Bw. Gift Shoko ambaye ni Afisa Mkurugenzi Mkuu wa benki ya CBA Tanzania ni mteule katika bodi ya benki ya NCBA kama Mtendaji Mkuu, na ameteuliwa kuiongoza taasisi mpya kama Mkurugenzi Mtendaji wa biashara za kidijitali na wateja wadogo na wakubwa

                                                                                         

Nafasi yake itaiongoza benki ya NCBA kwenye biashara za kidijitali ambapo ni kiini cha ukuaji endelevu wa biashara ya kundi hili wakati inalenga kuwa benki inayoongoza kwenye kanda katika miaka mitano ijayo.



"Kuleta benki zote mbili pamoja imetuwezesha kukua na kuwa benki kubwa katika sekta ya digitali. Kadri ambavyo teknolojia inaendelea kukua tunashuhudia teknolojia ikiwa inachukua nafasi muhimu zaidi katika kuleta ushirikishwaji wa kifedha nchini Tanzania, Afrika Mashariki na kwa bara zima kwa ujumla.  Tuna vifaa, rasilimali na wataalamu wa kutuwezesha kuongoza katika soko, "Alisema Bwana Shoko. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...