Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba (kushoto) akitembelea banda la TTCL katika Maoneshoya 44 ya Biashara Kimataifa ya Sabasaba akishuhudia bidhaa na huduma mbalimbali zinazotolewa katika banda hilo. 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba (kulia) akifanya mazungumzo ya moja kwa moja na maofisa wa TTCL Mkoa wa Dodoma kwa kutumia huduma ya 'Video Conference' inayotolewa na shirika hilo, alipotembelea banda la TTCL kwenye Maoneshoya 44 ya Biashara Kimataifa ya Sabasaba. 
Baadhi ya wateja wa TTCL (kushoto) wakipata huduma za usajili laini zao walipotembelea Banda la TTCL katika Maoneshoya 44 ya Biashara Kimataifa ya Sabasaba. 

Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limepeleka huduma yake maarufu ya ‘T-Burudani’ katika Maonesho ya 44 ya Biashara Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ndani ya Banda la TTCL, Meneja Uhusiano wa Shirika la Mawasiliano Tanzania, Bi. Puyo Nzalayaimisi alisema Watanzania watakaotembelea maonesho ya mwaka huu ndani ya banda lao, watajipatia huduma ya T-Burudani nyenye ofa ambayo inatamwezesha mteja kupakua, kuhifadhi pamoja na kuangalia filamu aipendayo hata bila ya kuwa na mtandao wa intaneti.


Aliwaomba wananchi hasa wapenzi wa filamu nchini kufurahia ofa hiyo ya shilingi 2000 tu na kujipatia huduma ya T-Burudani toka TTCL itakayomwezesha mteja kuangalia filamu na tamthilia aipendayo bila ya kuwa na mtandao wa intaneti.

Mfanyakazi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Emerco Mashelle (kulia) akimuhudumia mmoja wa wateja wa TTCL waliotembelea Banda lao katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam. 

“Huduma ya T-Burudani ya TTCL ni rahisi inamuwezesha mteja kupakua filamu bila kutumia kifurushi cha intaneti, mteja ataweza kuangalia filamu zote za ndani ya nchi pamoja na kimataifa, mteja ataweza kupakua kupitia simu janja ya mkononi pamoja na kompyuta ya kiganjani ‘Tablet’,” alisema Bi. Nzalayaimisi.

Aidha akifafanua zaidi juu ya huduma hiyo, alisema TTCL imeweka mfumo rahisi utakaomuwezesha, mteja kupakua filamu aitakayo kutokana na maudhui anuai duniani ikiwa ni pamoja na Hollywood, Nollywood, Bollywood, HBO, na Bongo movies.

Aliongeza huduma nyingine ambazo TTCL inazitoa katika viwanja vya Sabasaba ni pamoja na huduma za usajili laini kwa wateja, kurudisha laini zilizopotea,vifaa vya internet kama modem na vinginevyo, huduma za T-PESA, huduma za mkongo wa taifa wa mawasiliano na huduma za Data Senta.
Kushoto ni mmoja wa wateja akihudumiwa ndani ya banda la TTCL katika Maonesho ya 44 ya Biashara Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Sehemu ya wafanyakazi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), wanaotoa huduma ndani ya banda la TTCL kwenye Maonesho ya 44 ya Biashara Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...